* Mbwembwe,sherehe marufuku
*Idadi ya wadhamini, mikoa sasa yaongezwa
*Wajumbe NEC, marufuku kudhamini wagombea
*Idadi ya wadhamini, mikoa sasa yaongezwa
*Wajumbe NEC, marufuku kudhamini wagombea
Chama
cha Mapinduzi(CCM), kimetangaza rasmi ratiba ya kuchukua na kurejesha
fomu kwa ajili ya kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ikiwemo ya
urais, huku kikitoa masharti magumu kwa wanaotaka kuwania urais kupitia
chama hicho.
Chama hicho kimetoa msimamo
wake kuwa wagombea wanatakia kuheshimu kanuni na misingi ya chama hicho
na ni marufuku kwa wagombea kufanya mbwembwe, madoido na kukodi watu kwa
ajili ya kukushangilia wakati wa kuchukua fomu au kurudisha ni
marufuku.
Akitangaza uamuzi wa wajumbe wa
Halmashauri Kuu(NEC) ya chama hicho, leo mjini Dodoma,Katibu wa Itikadi
na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye amesema fomu ya kugombea urais itaanza
kutolewa Juni 3 mwaka huu na kuzidurisha Julai 2 mwaka huu saa 10 jioni.
Amesema kuanzia Juni 3
wanaruhusiwa kuanza kuchukua fomu na kuzirudisha Julai 2 mwaka huu.
Wakishachukua fomu watafanya kazi ya kutafuta wadhamini mikoani.
Amesema mwaka huu idadi ya
wadhamini imeongezeka kutoka wadhamini 250 hadi wadhamini 450 huku idadi
ya mikoa nayo ikiongezeka kutoka 10 hadi 15.
Nape amesema kuongeza kwa
wadhamini hao ni kutokana na idadi ya wanachama wao kuongezeka na wakati
huo huo mikoa nayo imeongezeka.Hivyo lazima wagombea waende kwenye
mikoa hiyo ambapo mikoa 12 kwa Tanzania Bara na mikoa mitatu Zanzibar na
moja ya mkoa uwe Pemba au Unguja.
Amesema moja ya sharti ni
kuhakikisha wadhamini wa mgombea mmoja wa ngazi ya urais hawatakiwi kuwa
wadhamini wa mgombe mwingine .Hivyo kila mdhamini mmoja anatakiwa
kumdhamini mgombea mmoja na si zaidi.
“Tumekubaliana kwenye NEC
mwanachama mmoja anatakiwa kumdhaminni mgombea mmoja tu.Haitaruhusiwa
mwachama mmoja kuwadhamini wagombea wawili.
Pia amesema wakati wa kuchukua
fomu na kurejesha ni marufuku mgombea kufanya mbwembwe za aina yoyote
huku akifafanua ni muhimu wagomba kusoma kanuni na kuzielewa mapema.
Kwa mujibu wa Nape ni kwamba
vikao vya uchuchaji ni kwamba Kamati ya Maadili na Usalama itachuja
majina ya wagombea urais Julai 8 mwaka huu, Kamati Kuu(CC) itachuja
majina Julai 9 mwaka huu na Halmashauri Kuu nayo itapitisha jina la
mgombea Urais Zanzibar.
Wakati kwa jina la mgombea
urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jina litapitishwa na wajumbe wa
Mkutano Mkuu Julai 11 mwaka huu mjini hapa.
Alisisitiza wagombea urais
wanatakiwa kuheshimu kanuni za chama hicho katika mchakato mzima wa
kuchukua fomu, kurudisha na hata wakati wa kutafuta wadhamini na mwaka
huu masharti yameongezeka kidogo likiwemo la idadi ya wadhamini na
wagombea kuhakikisha hawakiuki kanuni za maadili.
“Sharti ambalo limetolewa na
NEC ni kwamba marufuku wajumbe wa NEC na Kamati kuu kuwadhamini wagombea
urais kwani wao ndio watakaopitisha jina la mgombe, hivyo hawatakiwi
kua sehemu ya wadhamini.
.
Kuhusu kuchukua fomu ya
udiwani, ubunge na uwakilishi, Nape amesema fomu zitaanza kutotolea
Julai 15 mwaka huu na kurudishwa Julai 19 mwaka huu wakati mikutano ya
kempeni itaanza Julai 20 hadi Julai 31 mwaka huu.
Nape alisema kura ya maoni
itafanyika Agosti 1 mwaka huu wakati wabunge wa viti maalumu nayo
itakuwa Julai 15 mwaka huu na kurudisha fomu Julai 19 na kufafanua
uchujaji wa majina utafanywa na Jumuiya ya Umoja wa Wanawake(UWT), Taifa
licha ya kwamba mchakato wake utapita Baraza la Vijana.
Kwa
upande wa gharama za fomu kwa ajili ya kuwania nafasi mbalimbali za
uongozi kwenye chama hicho,Nape alisema fomu ya kugombea urais itakuwa
sh.milioni moja, wakati fomu ya kugombea ubunge ni sh.100,000 na fomu ya
udiwani sh.50,000.
Comments