- Get link
- Other Apps
Rais wa
Jamhuri ya Muugano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete
amewateua Majaji wawili wa Mahakama Kuu ya Tanzania kuwa Majaji wa
Mahakama ya Rufani kuanzia Jumamosi iliyopita, Aprili 24, 2015, taarifa
iliyotolewa Dar es Salaam, jana, Alhamisi, Aprili 30, 2025 na Ofisi ya
Katibu Mkuu Kiongozi (KMK) imesema.
Taarifa
hiyo imewataja wajaji hao kuwa ni Jaji Augustine Gherabast Mwarija na
Jaji Stella Ester Augustine Mugasha, ambao wote wamekuwa Majaji wa
Mahakama Kuu ya Tanzania tokea walipoteuliwa Novemba 28, 2006.
Kabla ya
uteuzi wake, Jaji Mwarija alikuwa Jaji Mfawadhi, Kitengo cha Biashara,
Mahakama Kuu, Dar Es Salaam. Kabla ya kuwa Jaji wa Mahakama Kuu alikuwa
Msajili wa Mahakama ya Rufani kati ya mwaka 2003 na 2006.
Aliajiriwa kama Hakimu Mkazi Daraja la Tatu Februari 2, mwaka 1987, baada ya kupata Shahada ya Sheria mwaka 1986.
Naye Jaji
Mugasha, kabla ya uteuzi wake, alikuwa Jaji Mfawidhi, Dar es Salaam.
Alikuwa Mfawidhi, Mahakama Kuu, Kanda ya Arusha na awali Kanda ya Moshi
tangu 2009 hadi alipohamishiwa Mahakama Kuu, Dar Es Salaam.
Aliajiriwa kama Wakili wa Serikali mwaka 1983 baada ya kupata Shahada ya Sheria mwaka huo huo, 1983.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
Comments