SHIGONGO AZINDUA VITABU VYAKE VITATU VIPYA KATIKA OFISI ZA GLOBAL



MHAMASISHAJI na mjasiriamali wa kimataifa, Eric James Shigongo, amewaasa Watanzania kutokata tamaa katika kufuatilia ndoto zao huku wakiamini kuwa wao ni watu muhimu katika maisha yao na ya jamii.

Akizungumza na vyombo vya habari mapema leo ndani ya ofisi za Global Publishers zilizoko Mwenge-Bamaga jijini Dar katika uzunduzi maalumu wa vitabu vyake vitatu, Shigongo aliwataka Watanzania kuwa na tabia ya kusoma vitabu ili kupata maarifa mengi ya juu ya mafanikio maishani.

 “Kila mmoja ana ndoto za kufikia malengo yake ikiwa ni pamoja na kuondoka mahali alipo. Wengi hushindwa kupiga hatua za mafanikio maishani kwa sababu nyingi yakiwemo mazingira waliyokulia wakiaminishwa kuwa hawawezi kufanya chochote maishani,  jambo ambalo si la kweli kwani kila mmoja anaweza kufikia ndoto zake akiamua tu kubadili fikra na namna ya kutenda mambo maishani,” alisema Shigongo.

Vitabu vilivyozinduliwa ni ‘Sheria 10 Zilizothibitishwa – Jinsi ya Kutoka Kwenye Umaskini Hadi Mafanikio’, cha pili ni ’10 Proven Secrets – How to Move From Poverty to Success’ na cha tatu ni  ’26 Secrets – How to Defeat Your Enemies and Make Millions of Dollars’.

Uzinduzi wa vitabu hivyo ni kuashiria kwake kuingia rasmi mitaani na kusambazwa kwenye kona mbalimbali ndani na nje ya nchi ambapo vinatarajiwa kubadilisha maisha ya maelfu ya wasomaji watakaofanikiwa kupata siri za mafanikio.
Mkurugenzi wa Global Publishers LTD, Shigongo Eric James (kulia), akishikilia vitabu vyake baada ya kumpatia jukumu la uzinduzi huo Mhariri Kiongozi wa Magazeti Pendwa ya Kampuni hiyo, Oscar Ndauka. Tukio hilo limefanyika mapema leo ndani ya jengo la ofisi za GlobalPublishers zilizoko Mwenge-Bamaga jijini Dar es Salaam.
Meneja Mkuu wa Global Publishers Ltd, Abdallah Mrisho (kulia), akiwa amenyanyua moja ya vitabu hivyo baada ya zoezi la kukata utepe wa uzinduzi kukamilika.  Katikati ni mtunzi wa kitabu hicho, Shigongo Eric James na Oscar Ndauka, wote wakiwa wamenyanyua vitabu hivyo. Vitabu vilivyozinduliwa ni ‘Sheria 10 Zilizothibitishwa – Jinsi ya Kutoka Kwenye Umaskini Hadi Mafanikio’, cha pili ni ’10 Proven Secrets – How to Move From Poverty to Success’ na cha tatu ni  ’26 Secrets – How to Defeat Your Enemies and Make Millions of Dollars’.
Shigongo akimkabidhi jukumu la kukata utepe Mhariri Kiongozi wa Magazeti Pendwa Oscar Ndauka (wa kwanza kushoto) huku Meneja Mkuu wa Kampuni hiyo Abdallah Mrisho anashuhudia zoezi hilo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*