Waziri wa Nishati na Madini,
George Simbachawene, akipokelewa na Wazee wa Kijiji cha Wangi na
Viongozi wa Chama na Serikali wa Wilaya ya Mpwapwa wakati wa ziara yake
kijijini hapo.
Waziri wa Nishati na Madini,
George Simbachawene akizizitiza jambo wakati akiongea na wananchi wa
Kijiji cha Wangi, Wilayani Mpwawa, Mkoani Dodoma kuhusu hatua
zilizofikiwa za Utekelezaji wa Mradi wa Umeme Vijijini Awamu ya Pili,
unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini REA na TANESCO.
Mtaalamu kutoka Wakala wa Nishati
Vijijini (REA), Kanda ya Kati , Mhandisi Michael Kessy akieleza jambo
kuhusu Mradi wa Umeme Vijijini unaotekelezwa na REA kwa kushirikiana na
Shirika la Umeme Nchini. (TANESCO). Wengine wanaomsikiliza ni Waziri wa
Nishati na Madini George Simbachawene na Wataalamu kutoka TANESCO.
Waziri wa Nishati na Madini,
George Simbachawene , akishauriana jambo na Wataalamu kutoka Wizara ya
Nishati na Madini, Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) (Kanda ya Kati) na
Mtaalamu kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA), wakati wa mkutano wa
hadhara katika Kijiji cha Lwihomelo wilayani Mpwapwa, Mkoani Ddodoma,
Waziri Simbachawene alifika kijijini hapo kuwaeleza wananchi kuhusu
hatua iliyofikiwa ya Utekelezaji wa Mradi wa Umeme Vijijini Awamu ya
Pili, katika eneo la kijiji hicho. Wengine ni Mwenyekiti wa Kijiji hicho
na Kiongozi wa CCM wilayani hapo
Waziri wa Nishati na Madini George
Simbachawene akisalimiana na baadhi ya Wazee wa Kijiji cha Wota wakati
akiwasili kijijini hapo kuongea na wananchi kuhusu hatua ya Utekelezaji
wa Mradi wa Umeme Vijijini , Awamu ya Pili kijijini hapo.
Waziri wa Nishati na Madini,
George Simbachawene (wa kwanza kushoto), akiwatambulisha Wataalamu
kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Shirika la Umeme Nchini (TANESCO),
na Wakala wa Nishati Vijijini (REA), ambao aifuatana nao katika ziara ya
kueleza utekelezaji wa Mradi huo katika kijiji cha Wota.
Mmoja wa wananchi katika kijiji
cha Lwihomelo, Wilayani Mpwapwa Mkoani Dodoma akiwasilisha kero ya
Kijiji kwa niaba ya wanakijiji kwa Waziri wa Nishati na Madini, George
simbachawene wakati wa ziara yake kijijini hapo.
Sehemu ya wananchi wa Kijiji
cha Wangi wakifuatilia mkutano wa hadhara wa wakati Waziri wa Nishati na
Madini, George Simbachawene alipotembelea kijijini hapo wakati wa ziara
yake ya kueleza hatua iliyofikiwa ya utekelezaji wa Mradi wa Umeme
Vijijini Awamu ya Pili katika Kijiji hicho.
…………………………………………………………………….
Na Asteria Muhozya, Mpwapwa-Dodoma
Wananchi wa Vijiji mbalimbali Wilayani Mpwapwa Mkoani Dodoma
vikiwemo vya Wangi na Lwihomelo, wametakiwa kutumia Umeme kwa shughuli
za kiuchumi wakati vijiji hivyo vitakapounganishwa na huduma hiyo badala
ya kutumia nishati hiyo kwa ajili ya mwanga tu.Simbachawene ameyasema hayo wakati wa ziara yake Wilayani Mpwapwa, Mkoani Dodoma wakati akieleza hatua mbalimbali zilizofikiwa katika kuviunganisha vijiji hivyo na huduma ya Umeme unaotokana na Utekelezaji wa Mradi wa Umeme Vijijini Awamu ya Pili, unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Nchini (TANESCO).
Aidha, ameongeza kuwa wananchi wanapaswa kuelewa kuwa nishati ya umeme ni kichocheo kikuu cha ukuaji uchumi hivyo, amewataka wananchi hao kuitumia nishati hiyo kwa kutengeneza ajira mbalimbali zinazotokana na nishati hiyo.
“Kumbukeni kwamba Serikali inatumia fedha nyingi katika miradi hii, lakini vilevile miradi hii ni uwekezaji mkubwa hivyo, tumieni umeme katika shughuli za kiuchumi zitazowezesha kuchangia gharama za uwekezaji huu mkubwa kupitia shughuli zenu.
Vilevile, katika ziara hiyo, Waziri Simbachawene amewaasa wananchi hao kuandaa mazingira ya nyumba bora zitakazokuwa na viwango vya kupokea nishati hiyo. “Andaaeni nyumba zenu na mazingira wakati mnasubiri kuunganishwa na nishati hii”, amesema Simbachawene
Comments