WAZIRI WA AFYA AIPONGEZA MUHIMBILI KUFANIKISHA MATIBABU YA MOYO KWA WATANZANIA

 Mh. Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Seif Rashid akimjulia hali leo baada ya kufanyiwa upasuaji. Kushoto kwake ni mama Catherine akifurahia baada ya mtoto wake kufanyiwa upasuaji.
 Mtoto Michelle Colila (5) akifurahi baada kusalimiwa na Mh. Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Seif Rashid ambapo pembeni yake ni mama Michelle.
 Mtoto Cherish Chatama akifurahi baada kusalimiwa na Mh. Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Seif Rashid ambapo pembeni yake ni mama Cherish
 Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Seif Rashid akiwa na mtoto ambaye anasubiri kufanyiwa uchunguzi wa kina kama anahitaji upasuaji wa moyo au la.
 Hapa ni ndani ya chumba chenye vifaa vya kisasa kabisa kwa ajili ya wagonjwa wenye kuhitaji uangalizi maalumu (ICU) ambapo mtoto aliyefanyiwa upasuaji anaangaliwa.
 Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Seif Rashid ambapo kulia kwake ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Dkt. Hussein Kidanto wakiwa ndani ya Chumba chenye mtambo wa Cath Lab ambao unatumika kuzibua mishipa ya damu inayopeleka damu kwenye moyo iliyoziba na pia mtambo huu pamoja na mambo mengine umetumika kwa mara ya kwanza kuziba matundu ya moyo bila kufungua kifua. Mtoto huyu ambaye jina lake limehifadhiwa anasubiri kuzibwa tundu kwenye moyo wake kwa kutumia mtambo wa Cath Lab. Ndani ya siku tatu ataruhusiwa kwenda nyumbani.
 Jopo la wataalam wakiwa ndani ya chumba cha kisasa cha upasuaji moyo wakiendelea na upasuaji moyo.
 Jopo la Watalaam wakifurahi baada ya kumaliza upasuaji kwa ufanisi na mgonjwa kupelekwa chumba maalumu (ICU).
mtoto Catherine Gwabala (6) alikuwa wodini jumamosi iliyopita akisubiri kufanyiwa upasuaji.
---
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Mh. Dkt. Seif Rashid ameipongeza Hospitali ya Taifa Muhimbili kupitia Idara yake ya Tiba na Upasuaji Moyo kwa kufanikisha matibabu ya moyo kwa wagonjwa 24 katika kipindi cha siku nne. 

Hayo ameyasema alipotembelea Hospitali hiyo kuona namna ambavyo wataalam wetu kwa kushirikiana na madaktari bingwa kutoka Hospitali ya Prince Sultan Cardiac Centre iliyoko Riyadhi nchini Saudi Arabia ambao wamekuwepo Muhimbili toka tarehe 9 Mei na wanatarajiwa kuondoka tarehe16 Mei, mwaka huu.

Dkt. Rashid amesema ni mfanikio makubwa sana ambayo tumefikiwa hadi hivi sasa katika upasuaji moyo na tunatarajia kasi hii ya ushirikiano ikiendelea tutapunguza kwa kasi sana wagonjwa wanaopelekwa nje ya nchi kwa ajili ya matibabu.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*