NAWERA AITAKA WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII KUPUNGUZA BEI KUBWA ZA DAWA NCHINI



Elias Nawera
Na Dotto Mwaibale

MWENYEKITI wa Chama cha Walaji na Tiba Tanzania , Elias Nawera, ameitaka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kutatua changamoto ya bei kubwa ya dawa za binadamu wanayotozwa Watanzania.

Nawera alisema sera ya afya inasema kila mtu ana haki ya kupata huduma za afya kwa bei nafuu, lakini bado Watanzania wengi wanakabiliwa na changamoto kubwa ya kununua dawa kwa bei kubwa.
“Tunaomba Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii aingilie kati suala hili,
wanaoteseka kwa kiwango kikubwa ni watu wa kipato cha chini.

Nimesema hivi baada ya Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) na Baraza la Famasia kushindwa kulitafutia ufumbuzi suala hili.

Alitoa kauli hiyo Dar es Salaam juzi, wakati akizungumza na wanahabari, ambapo alifafanua kuwa, amefikia hatua hiyo baada ya kubaini mzigo mkubwa wa gharama za matibabu wanaobebeshwa Watanzania.

Aidha, Mwera alisema kupanda kwa gharama za dawa hakuna uhusiano wowote na kupanda kwa gharama za maisha na kwamba, wizara husika ikifuatilia inaweza kulipatia ufumbuzi suala hilo.(Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA