BARAZA LATAIFA LA UWEZESHAJI NA BENKI YA POSTA WASAINI MAKUBALIANO KUWAINUA WANA VIKOBA KIUCHUMI

Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, (NEC), Beng’ Issa, (kushoto), Mkurugenzi Mkuu wa Benjki ya Posta, Sabasaba Moshingi, (wapilia kulia), Rais wa VICOBA Endelevu Tanzania, Devota Likokola, (wapili kushoto), Mwanasheria wa Benki ya Posta Tanzania, Mystica Mapunda Ngongi, (wakwanza kulia), wakiwa wameshikana mikono baada ya benki hiyo kutiliana saini makubaliano ya ushirikiano kati ya baraza na benki hiyo, katika kuwawezwesha wana VICOBA kiuchumi. Hafla hiyo ilifanyika leo Julai 14, 2015. kwenye ukumbi wa wizara ya fedha jijin I Dar es Salaam.
 BARAZA la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, (NDC), na Benki ya Posta Tanzania, (TPB), wamesaini makubaliano ya ushirikiano wa kuwawezesha wanachama wa VCOBA nchini.

Akizungumza wakati wa hafla ya kutiliana saini makubaliano nhayo kwenye ukumbi wa wizara ya fedha jijini Dar es Salaam leo Julai 14, 2015, Katib u Mtendaji wa baraza hilo, Beng’ Issa, alisema, Katika juhudi za kuwawezesha watanzania kiuchumi kupitia upatikanaji wa mitaji na kuendeleza ujasirimali nchini, Serikali kupitia Sheria ya Taifa ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi ya mwaka 2004, ibara ya IV, sehemu ya 16  iliagiza  uanzishwaji wa Mfuko wa Taifa wa Uwezeshaji Mwanachi yaani ‘’Mwananchi Empowerment Fund,”.

“Katika kukabiliana na changamoto ya ukosefu wa mitaji yenye gharama nafuu kwa wajasiriamali nchini, Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi limesaini hati za makubaliano na Benki ya Posta Tanzania katika kusimamia udhamini wa mikopo  yenye masharti nafuu kwa makundi  mbali mbali  ya wajasiriamali nchini yanayokidhi masharti husika.” Alisema Beng’i.

Mfuko huu utakao simamiwa na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi ni pamoja na kutoa fursa kwa wananchi katika makundi au mtu mmoja mmoja kupata mitaji ya kuwekeza kwenye miradi ya kiuchumi kupitia mikopo ya moja kwa moja au udhamini (direct lending   or guarantee system).

Ili kutimiza azama hiyo baraza limeamua kushirikiana na benki ya ;posta Tanzania ambayo ina mtandao mpana, kutekeleza azma hiyo ambapo wananchama wa VICOBA, watapata mikopo na mafunzo kutoka benki ya posata.

Kwa aupande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Posta, Sabasaba Moshingi, alisema, benki yake  ni benki ya wananchi na hivyo unayo furaha kubwa kushirikiana na NE, ili kuwakwamua wananchi kiuchumi kwa kupata mikopo itakayowazsaidia kuendesha shughuli zao za kiuchumi.
“Benki ya Posta inayo furaha kubwa kushirikiana na Baraza hili ili kuwawezesha wananchi wengi zaidi kupata huduma za kifedha kwa gharama nafuu kupitia mpango huu.” Alifafanua Moshingi.

Alisema, Benki ya Posta inaamini kuwa hii ni fursa muhimu kwa vikundi hivi visivyo rasmi  kufungua akaunti na kuweka fedha zao mahala salama. Hili litawawezesha kufanya shughuli zao kwa ufanisi zaidi, na hatimaye wataweza kupatiwa mikopo nafuu kwa ajili ya kukuza biashara zao. Hadi sasa Benki imefungua zaidi ya akaunti 340 za vikundi. Vikundi hivi vitafaidika pia na huduma ya TPB POPOTE, itakayo wawezesha kupata huduma za kifedha popote pale walipo.



 Katibu Mtendaji wa NDC, Beng'i Issa

 Mkurugenzi Mtendajin wa TPB. Sabasaba Moshingi
 Moshingi, (kulia), Beng'i(katikati) na Lokokola, wakibadilishana mawazo mwishoni mwa hafla hiyo

 Devota akishukuru Mungu, baada ya kufikiwa makubaliano hayo ambapo wanachama wake ni wafaidika wakubwa
 Picha ya pamoja, Viongozi wa TPB, NDC, na Vicoba endelevu, wakiwa katika picha ya pamoja na waliohudhuria hafla hiyo


Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*