JESHI LA POLISI LATOA TAHADHARI ZA KIUSALAMA SIKUKUU YA IDD

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI
JESHI LA POLISI TANZANIA


Anuani ya simu “ mkuupolisi”                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                               Ofisi ya  Inspekta  Jenerali wa Polisi,
Simu : (022) 2110734                                                                                            Makao Makuu ya Polisi,
Fax na. (022) 2135556                                                                                                           S.l.P. 9141,
Unapojibu tafadhali taja:                                                                                    Dar es Salaam.

          


                                                    16/07/ 2015

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Tunaelekekea kipindi hiki cha kusherehekea sikukuu ya Eid-El-Fitr na ambapo wananchi wenye imani ya kiislam na hata madhehebu mengine hutumia muda huo kwenda kuabudu pamoja na muendelezo wa sherehe hizo kwenye maeneo mbalimbali ya starehe, Jeshi la Polisi nchini linatoa wito kwa wananchi wote kuwa makini na kusheherekea sikukuu hiyo kwa amani na utulivu pasipo vitendo ama viashiria vyovyote vya uvunjifu wa amani.

Jeshi la Polisi nchini linapenda kuwaondoa hofu wananchi kuwa, limejipanga vizuri kuhakikisha wananchi wanasherehekea sikukuu hiyo kwa amani na utulivu. Ulinzi umeimarishwa kwenye maeneo yote ya kuabudia, fukwe za bahari, sehemu za starehe na maeneo mengine yote.

Aidha,  tahadhali zichukuliwe kwa wale wote ambao watakuwa wakitumia barabara ikiwemo maderera na watembea kwa miguu, kuwa makini kwa kuzingatia sheria za usalama barabarani na hasa kwa madereva wa magari na pikipiki kuepuka kwenda mwendo kasi na kutumia vilevi wawapo kazini.

Jeshi la Polisi linaendelea kuwasisitiza wananchi kutoa taarifa haraka kwenye vyombo vya dola juu ya kitu chochote ama mienendo ya watu watakaowatilia shaka mahali popote kwani taarifa hizo za haraka zitasaidia kuzuia uhalifu kabla haujatokea.

Vilevile wananchi wachukue tahadhari watokapo kwenye makazi yao, wasiache nyumba wazi ama bila mtu na endapo italazimika basi ni vema watoe taarifa kwa majirani zao kwa ajili ya usalama.

TUNAWATAKIA WATANZANIA WOTE SIKUKUU NJEMA YA EID –EL-FITR

Imetolewa na:
Advera John Bulimba-SSP
Msemaji wa Jeshi la Polisi

Makao Makuu ya Polisi.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI