Picha ya 1-2 ni mmoja wa watu
wanaodaiwa kuwa ni majambazi akiwa mikononi mwa polisi baada ya kutiwa
mbaroni Mnara wa Saa maeneo ya Stesheni Dar es Salaam leo mchana kwa
madai ya kupora kiasi kikubwa cha fedha. Watu hao wanadaiwa kuwa
walikuwa wanne.
Kijana mwingine anayedaiwa kuwa ni jambazi akiwa amekamatwa.
Watuhumiwa hao wanne wa ujambazi wakiwa ndani ya Noah kabla ya kupelekwa Kituo Kikuu cha Polisi. Kulia ni askari Polisi.
Askari kanzu (katikati), ndiye anadaiwa
kuwadhibiti majambazi hayo kabla ya kujificha chini ya uvungu wa taxi
zinazoegeshwa jirani na Mnara wa Saa katika makutano ya barabara ya
Uhuru, Samora na Nkruma.
Gari lenye namba T 976 BKK walilokuwa wakitumia majambazi hayo liondolewa eneo la tukio kupelekwa kituo kikuu cha polisi.
Wananchi wakiwa eneo la tukio.
Askari Polisi wakilipekua gari walilokuwa wakitumia watu hao wanaodaiwa kuwa ni majambazi.
Upekuzi ukiendelea.
Maofisa wa polisi wakiteta jambo eneo la tukio baada ya kuwakamata majambazi hayo. (Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com)
Comments