Kipindi cha pili kilianza kwa kasi ambapo Barca waliweza kuonesha kumiliki mpira kwani waliweza kupiga pass 314 kwa 198 huku zikiwa zenye asilimia 90.8 dhidi ya zile 80.8 za Manchester United.
Manchester United Usiku wa Kuamkia jumapili ya tarehe 26/7/2015 waliweza kuandika historia katika Mchezo wa soka kwa kucheza Mechi na Magwiji wa soka kutoka Hispania timu ya Barcelona na Hadi kupyenga cha Mwisho ni Machester United iliyoibuka kidedea kwa Ushindi mnono kabisa wa Mabao 3 - 1 dhidi ya Barcelona.
Ni Manchester United ambao walikuwa wakwanza kuandika bao la Kwanza mnamo dakika ya 8 ya mchezo huo kupitia kwa Mchezaji Wayne Rooney ambaye alifunga Goli hilo baada ya Mpira wa Kona kupigwa na Ashley Young na Kumkuta yeye na kupiga Kichwa safi kabisa na kumuacha Mlinda mlango wa Barcelona Ter Stegen akishindwa kuokoa Mchomo huo.(P.T)
Comments