OBAMA AWASILI KENYA

Rais Barack Obama
Rais Barrack Obama wa Marekani, tayari amewasili mjini Nairobi.
Ndege iliyombeba rais obama ilitua katika uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta muda mfupi baada ya saa mbili za usiku.
Alipowasili Rais Obama amelakiwa na mwenyeji wake Rais Uhuru Kenyatta.
mwendo wa saa mbili na robo rais Obama alitua ndege yake.
Akisalimiana na ndugu zake
Alipowasili alizungumza kwa muda mfupi na mwenyeji wake rais Kenyatta na kisha kutia saini kitabu cha wageni kabla ya kuondoka.
Obama sasa ameandikisha historia ya kuwa rais wa kwanza wa Marekani, kuzuru Kenya akiwa ofisini.
Obama anatarajiwa kufungua mkutano wa sita wa kimataifa kuhusu ujasiriamali katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini Nairobi.
Ndege ya Obama katika Uwanja wa JKIA
Baadaye rais huyo atafanya mashauriano na rais Uhuru Kenyatta katika ikulu ya Nairobi.
Siku yan Jumapili rais Obama atahutubia mkutano wa wakuu wa mashirika ya kijamii katika chuo kikuu cha Kenyatta kabla ya kuhutubia mkutano mwingine kwa wakenya wote katika uwanja wa Kasakani.
Obama anatarajiwa kuondoka siku ya Jumapili kuelekea nchini Ethiopia.
Maelfu ya wakenya wamejipanga kando ya barabara kuu inayotoka uwanja wa ndege ili kumlaki rais huyo wa Marekani, ambaye anarejea nchini Kenya ambako babake alizaliwa.
Wakenya wakifuatilia ziara ya Obama kwenye runinga
Mamilioni ya Wakenya wengine naowalifuatilia kuwasili kwake kwenye runinga.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI