Kulikuwa
na stori ya uzushi mitandaoni na June 24 nikamfata nyumbani kwao Sinza
na kwenye majibu yake kulikuwa na hiki ambacho nilimnukuu pia
>>>> ‘Sio mara ya kwanza
kuzushiwa kifo, nasikia mara watu oooh banza kafa, mara ooh kila mtu
anaongea lake ila mimi niko poa ni mzima… naweza kufanya kazi ila kwa
sasa siko tayari kufanya kazi kwani nitauchosha mwili wangu’
Hiyo haikuwa mara ya kwanza Banza Stone
kuzushiwa kifo.. muda mfupi baadae ikaja taarifa nyingine kwamba
mwimbaji huyo ambaye alikuwa ni legend wa Muziki wa dansi Tanzania
amelazwa katika Hospitali ya Mwananyamala Dar baada ya hali yake kuwa
mbaya.
Leo imetufikia nyingine, ni majonzi kwa kila mtu iliyemfikia taarifa hii, Banza Stone amefariki na hizi ni picha kutoka msibani, nyumbani kwa akina Banza Stone maeneo ya Sinza Kijiweni Dar es Salaam
Comments