Makamu
Mkuu wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam Profesa Rwekaza Mukandala
akimkabidhi Rais Dkt .Jakaya Mrisho Kikwete cheti cha Shahada ya Heshima
ya Doctor of Laws(Honoris Causa) wakati wa hafla fupi ya kumkabidhi
Rais joho na cheti iliyofanyika ikulu jijini Dar es Salaam na
kuhudhuriwa na maprofesa waandamizi wa chuo hicho.Tayari Rais Kikwete
alishatunukiwa shahada hiyo katika mahafali ya 41 ya UDSM yaliyofanyika
Octoba mwaka 2011.
Profesa
Agnes Mwakaje wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam akimvika kofia ya
kitaaluma Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa hafla fupi ya
kumkabidhi Rasmi Rais Joho na cheti cha shahada ya heshima ya Doctor of
Laws(Honoris Causa) ikulu jijini Dar es Salaam leo.
Makamu
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Profesa Rwekaza Mukandala akisoma
maelezo mafupi baada yeye na jopo la maprofesa waandamizi wa chuo hicho
kumkabidho Joho la taaluma na cheti cha Shahada ya heshima ya Doctor of
Laws(Honoris Causa) ya chu kikuu cha Dar es Salaam wakati wa hafla
iliyofanyika ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais
Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Makamu Mkuu wa
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Profesa Rwekaza Mukandakla pamoja na
maprofesa waandamizi wa chuo hicho muda mfupi baada hafla fupi ya
kumkabidhi Rais Joho na Cheti cha Shahada ya Heshima ya Doctor of
Laws(Honoris Causa) ikliyofanyika ikulu jijini Dar es Salaam leo(picha
na Freddy Maro)
Comments