Rais
Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akipokea hundi ya malipo ya Bima ya
Maisha(Flexi Provider) kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Bima la
Taifa(National Insurance Corporation of Tanzania Limited) NIC Bwana Sam
Kamanga Ikulu jijini Dar es Salaam leo.
Akimkabidhi hundi hiyo, Bw. Sam Kamanga amesema uwepo wa Mheshimiwa Rais kama mteja wa NIC imesaidia kukuza uelewa na shughuli za shirika hilo.
“Kitendo
cha Serikali kukatia Bima mali zake na taasisi zake, kumeongeza uwezo
wa kifedha wa shirika na soko la Bima” amesema na kuwataka watu binafsi,
taasisi mbalimbali na mashirika ya kiserikali kukata Bima kwa ajili ya
maendeleo na akiba ya baadaye.
Rais
Kikwete ameitaka NIC kuongeza juhudi katika kuhamasisha na kuelimisha
watanzania umuhimu na manufaa makubwa yanayopatikana kutokana na Bima.
Picha na Freddy Maro
Comments