URAIS CCM: TANO NA TATU BORA KUPATIKANA LEO

Jul 10, 2015

Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye ametoa ratiba ya Vikao kwa siku ya leo tarehe 10/7/2015.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Nape amesema, kuanzia Saa 4  hadi saa 7 mchana, kitafanyika kikao cha Usalama na Maadili chini ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete.

Amesema kuanzia Saa 8 hadi saa12 Jioni ni Kikao cha Kamati Kuu kitakachopitisha majina matano ya wagombea walioomba ridhaa ya CCM kuwania Urais.
 

Nape amesema na Saa 2 usiku baada ya waliofunga Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kufuturu, kitafanyika
Kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC), kwa ajili ya kupitisha majina matatu ili Mkutano Mkuu utakaoanza kesho asubuhi upokee majina hayo na kumchagua mmoja wapo atakayepeperusha bendera ya Chama.

SABABU YA KUCHELEWA VIKAO NA HASA KUTOFANYIKA JANA:

Nape amesema ratiba ya vikao ambayo ilikuwa imetolewa awali haikufuatwa kwa sababu ya Shughuli zilizojitikeza za Mhe Rais za Kichama na Serikali ambazo amekuwa akizifanya tangu alipowasili Dodoma juzi.

Amesema, sababu nyingine ni kuwepo kwa Vikao vya mashauriano, ili kuhakikisha kuwa vikao vya mchujo vinaisha kwa salama na hatimae Mgombea wa CCM apatikane kwa Amani.

 Baadhi ya waandishi wa habari waliopo mjini Dodoma, wakiirusha taarifa hiyo baada ya kuipata, leo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI

KOCHA WA AL.AHLY ASEMA YANGA NI TIMU BORA NA NGUMU