WAANDISHI WA HABARI KUTOKA VYOMBO MBALIMBALI WAKISUBIRI JINA LA MGOMBEA URAIS KUPITIA UKAWA USIKU HUU
Afisa
Habari wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema),Tumaini Makene
akizungumza na waandishi habari hivi punde juu kinachoendelea katika
mkutano wa kutafuta mgombea wa Urais kwa tiketi ya UKAWA, uliofanyika
katika Hoteli ya Colesseum jijini Dar es Salaam,Makene amesema
majadiliano hayo sio urais tu bali kuna mipaka ya majimbo mapya jinsi
watavyojipanga katika kushiriki uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 25
mwaka huu. Makene
amezidi kuwataka waandishi wawe na subira kusubiri maamuzi yatakayotoka
katika kikao hicho ambacho kimeanza tangu asubuhi ya leo.
Baada
ya kusubiri kwa muda mrefu tangu mchana,Waandishi wa Habari waliopiga
kambi wakisubiri kupata jina la mgombea Urais kwa tiketi ya UKAWA katika
Hoteli ya Colosseum Masaki leo jijini Dar es Salaam,wakajikuta wanaacha
stendi za Camera zao na kukaa pembeni kama zionekanavyo pichani usiku
huu,wakisubiri lolote litakalojiri.
Waandishi
wa Habari wakiwa wameweka kambi tangu saa saba mchana wakisubiri kupata
jina la mgombea urais kwa tiketi ya UKAWA katika Hoteli ya Colosseum
Masaki leo jijini Dar es Salaam, hiyo inatokana na taarifa zilizotolewa
na UKAWA kuwa leo ndio siku rasmi ya kutangaza jina hilo lakini masaa
yanazidi kwenda huku kikao chao kikiwa kinaendelea.
Waandishi
wakisubiri mtu wa kutoa taarifa juu ya jina la mgombea urais kwa tiketi
ya UKAWA, ambapo taarifa hizo za kuja mtu huyo ziligonga mwamba na
kuambiwa kilichobaki ni makubaliano suala jinsi kuendesha uchaguzi
katika majimbo.
Waandishi
wakijadiliana masuala yanayohusu tasinia ya habari baada muda mrefu
kuletewa jina la mgombea urais kwa tiketi ya UKAWA katika mkutano wao
uliofanyika katika Hoteli ya Colesseum ,Masaki jijini Dar es Salaam.
Waandishi wakiwa katika viyunga vya hoteli ya Colesseum wakisubiri jina la mgombea urais kwa tiketi ya UKAWA
Waandishi
wakiwa wamechoka na ucovu wa kusubiri jina la mgombea urais kwa tiketi
ya UKAWA katika Hoteli ya Colesseum leo jijini Dar es Salaam.
Comments