Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo
ya Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw.
James Kajugusi akiongea na Maafisa Vijana waliohudhuria Mfunzo ya
Ujasiriamali na Ubunifu kutumia elimu na uzoefu watakaoupata katika
mafunzo hayo kuwainua vijana kiuchumi kwa kutoa elimu itakayowajenga na
kuwafanya vijana kujitegemea na kuwa wajasiriamali, wakati wa ufunguzi
wa mafunzo hayo leo Jijini Arusha. Kulia ni Mkurugenzi wa Ujasiriamali
na Ubunifu kutoka Chuo cha Uongozi cha ESAMI (Eastern and Southern
Africa Management Institute) Bw. Leon Malisa.
Baadhi ya Maafisa Vijana
wakimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara
ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. James Kajugusi wakati wa
Ufunguzi wa Mafunzo hayo
Mkurugenzi Msaidizi kutoka Idara
ya Habari (MAELEZO) Bi. Zamaradi Kawawa akiwaeleza jambo Maafisa Vijana,
wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya Ujasiriamali na Ubunifu yaliyoandaliwa
kwa ushirikiano wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo na
Chuo cha Uongozi cha ESAMI (Eastern and Southern Africa Management
Institute)leo Jijini Arusha.
Mkurugenzi wa Ujasiriamali na
Ubunifu kutoka Chuo cha Uongozi cha ESAMI (Eastern and Southern Africa
Management Institute) Bw. Leon Malisa akiongea na Maafisa Vijana na
kuwataka kushiriki kikamilifu katika mafunzo ya Ujasiriamali na Ubunifu
yanayotolewa kwa ushirikiano wa Chuo hicho na Wizara ya Habari, Vijana,
Utamaduni na Michezo ili kuweza kuendeleza na kukuza ujasiriamali hasa
kwa Vijana, wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo leo Jijini Arusha.
Mkurugenzi wa Ujasiriamali na
Ubunifu kutoka Chuo cha Uongozi cha ESAMI (Eastern and Southern Africa
Management Institute) Bw. Leon Malisa akiongea na Maafisa Vijana na
kuwataka kushiriki kikamilifu katika mafunzo ya Ujasiriamali na Ubunifu
yanayotolewa kwa ushirikiano wa Chuo hicho na Wizara ya Habari, Vijana,
Utamaduni na Michezo ili kuweza kuendeleza na kukuza ujasiriamali hasa
kwa Vijana, wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo leo Jijini Arusha.
Baadhi ya Maafisa Vijana wakiwa
katika mijadala wakati wa mafunzo ya Ujasiriamali na Ubunifu
yaliyoandaliwa kwa ushirikiano wa Wizara ya Habari,
Baadhi ya Maafisa Vijana wakiwa
katika mijadala wakati wa mafunzo ya Ujasiriamali na Ubunifu
yaliyoandaliwa kwa ushirikiano wa Wizara ya Habari,Vijana, Utamaduni na
Michezo na Chuo cha Uongozi cha ESAMI (Eastern and Southern Africa
Management Institute)leo Jijini Arusha.
PICHA NA HASSAN SILAYO-MAELEZO
…………………………………………………………………………
Maafisa Vijana Nchini wametakiwa
kutumia elimu wanayopata katika kuwaendeleza vijana kiuchumi ili
kuwawezesha kushiriki katika shughuli za uzalishaji mali.
Hayo yamesemwa leo Jijini Arusha
na Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara ya Habari,
Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. James Kajugusi wakati wa Ufunguzi wa
awamu ya kwanza ya mafunzo ya Ujasiriamali na ubunifu.
Bw. Kajugusi alisema kuwa kwa
kutambua umuhimu wa kuwaendeleza vijana nchini Wizara kwa Kushirikiana
na Chuo cha Uongozi cha Mashariki na Kusini mwa Afrika (ESAMI)
wameanzisha mradi unaolenga kuwawezesha vijana kijasiriamali nakiubunifu
kwa kupitia mafunzo wanayowapa Maafisa Vijana.
“tunawaomba kushiriki kikamilifu
katika mafunzo haya ya ujasiriamali na ubunifu kwa kuwasikiliza
wawezeshaji kwa makini kwa dhumuni la kutumia elimu hiyo kuwainua vijana
nchini kiuchumi na kuwawezesha kushiriki kikamilifu katika
ujasiriamali”. Alisema Kajugusi.
Naye Mkurugenzi wa Ujasiriamali
na Ubunifu kutoka Chuo cha Uongozi cha Mashariki na Kusini mwa Afrika
(ESAMI) Bw. Leon Malisa alisema kuwa dhumuni la mafunzo haya ni
kuwajengea uwezo Maafisa Vijana katika eneo la ujasiriamali na ubunifu
ili kuwawezesha kuitumia Elimu hiyo kwa vijana vijana nchini kwa
kuwawezesha kujiajiri wenyewe.
Aidha Bw. Malisa ametaka vijana
nchini kuunda vikundi na kubuni miradi itakayowaendeleza ili Wizara kwa
kushirikiana na ESAMI waweze kuwasaidia kujiendeleza ikiwa ni njia moja
wapo ya kukabiliana na tatizo la Ajira Nchini.
Akizungumzia kuhusu mafunzo hayo
Afisa Vijana toka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw.
Eliackim Mtawa alisema kuwa watatumia mafunzo haya kuwatayarisha vijana
kuwa wajasiriamali wazuri na kuwasimamia katika utekelezaji wa Miradi
hiyo ili kuwawezesha kushiriki katika uzalishaji mali na kukuza uchumi
kupitia ujasiriamali
Mafuzno hayo ya Ujasiriamali na
Ubunifu yameandaliwa kwa ushirikiano wa Wizara ya Habari, Vijana,
Utamaduni na Michezo na Chuo cha Uongozi cha Mashariki na Kusini mwa
Afrika (ESAMI)
Comments