Zantel yatoa msaada wa vyakula kwa jumuiya ya wazee wa Zanzibar

1
Naibu Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazee Zanzibar (JUWAZA), Mwadini Kutenga akiwakaribisha wageni wakati wa shughuli ya makabidhino ya msaada wa chakula kutoka kwa Zantel kwenda kwa jumuiya ya wazee Zanzibar. Kulia kwake ni NAIBU Katibu Mkuu, Wizara ya Uwezeshaji, Ustawi wa Jamii , Vijana , Wanawake na Watoto, Nd. Msham Juma Khamis akifuatiwa na Mkurugenzi wa Biashara wa Zantel, Mohamed Mussa.
2Mkurugenzi wa Biashara wa Zantel, Mohamed Mussa akizungumza wakati wa makabidhiano ya msaada wa chakula kutoka Zantel kwa Jumuiya ya Wazee Zanzibar. Anayemfuatia ni NAIBU Katibu Mkuu, Wizara ya Uwezeshaji, Ustawi wa Jamii ,Vijana , Wanawake na Watoto, Nd. Msham Juma Khamis na mwisho ni Naibu Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazee Zanzibar (JUWAZA), Mwadini Kutenga.
3NAIBU Katibu Mkuu, Wizara ya Uwezeshaji, Ustawi wa Jamii , Vijana , Wanawake na Watoto, Nd. Msham Juma Khamis akimkabidhi msaada , Pili Ahmada wakati wa makabidhiano ya msaada wa vyakula uliotolewa na Kampuni ya simu ya Zantel kwa wazee mbali mbali wa Zanzibar, kulia Mkurugenzi wa Biashara wa Zantel Zanzibar, makabidhiano hayo yalifanyika jana Kibanda maiti.
5
NAIBU Katibu Mkuu, Wizara ya Uwezeshaji, Ustawi wa Jamii , Vijana , Wanawake na Watoto, Nd. Msham Juma Khamis akizungumza na wazee wakati wa kupokea msaada wa vyakula kutoka Zantel, kulia kwake ni  Mkurugenzi wa Biashara wa Zantel, Mohamed Mussa na kushoto ni Naibu Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazee Zanzibar (JUWAZA), Mwadini Kutenga.
6
Sehemu ya wazee waliokabidhiwa msaada wa vyakula na Zantel.
…………………………………………………………………….
Na Mwandishi wetu-Zanzibar
Kampuni ya simu za mikononi ya Zantel leo imetoa msaada wa vyakula kwa ajili ya mwezi wa Ramadhani kwa makundi maalumu ya wazee hapa visiwani Zanzibar.
Msaada huo unajumuisha sukari, unga wa ngano pamoja na mchele umetolewa katika hafla fupi ya makabidhiano iliyofanyika leo.
Kampuni ya Zantel upande wa Zanzibar imeainisha wazee zaidi ya 120 wenye uhitaji wa vyakula kwenye mwezi huu wa Ramadhani walio chini ya jumuiya ya wazee hapa Zanzibar.
Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo kwa wazee, Mkurugenzi wa Biashara wa Zantel-Zanzibar, bwana Mohammed Mussa, amesema ni kawaida kwa kampuni ya Zantel kusaidia makundi mbalimbali ya kijamii katika kipindi hiki cha Ramadhani.
‘Tuna furaha sana leo kuweza kusaidia jamii hii ya wazee ambao mara nyingi wamekuwa wanasahaulika, kwani tunaamini wazee ni sehemu muhimu sana ya jamii ndio maana Zantel leo tumeamua kutoa msaada huu ambao unatutofautisha sana na makampuni mengine katika vipaumbele vyetu’ alisema Mussa.
Mussa aliongeza kuwa kama kampuni ya simu inayoongoza Zanzibar, Zantel mara zote imekuwa mfano katika shughuli zake za kijamii na vipaumbele vyake kiujumla.
Akizungumza wakati wa shughuli hiyo, mgeni rasmi ndugu Msham Abdallah, ambaye ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ustawi wa Jamii Zanzibar, alisema anaipongeza Zantel kwa kushirikiana na serikali kuyasaidia makundi ya wazee.
‘Serikali imekuwa ikifanya juhudi mbalimbali katika kulisaidia kundi hili la wazee, kwahiyo ni furaha kwetu leo kuona Zantel imekuwa ya kwanza kusaidia kundi hili leo’ alisema bwana Abdallah.
Akitoa neno la shukrani kwa kampuni ya Zantel, naibu mwenyekiti wa jumuiya ya wazee Zanzibar, Bwana Mwadini Kutenga, alisema anawashukuru Zantel kwa msaada huo, akisema umekuja kwa wakati mufaka hasa ukizingatia kuwa wanakaribia kuadhimisha sikukuu ya Idi.
‘Kwa misaada hii, Zantel inawafanya wazee nao wajiskie sehemu ya jamii, kwani mara nyingi wamekuwa wakisahaulika sana na kwa hakika hatutawasau kwa ukarimu wao huu’ alisema bwana Kutenga.
Kampuni ya Zantel imekuwa msitari wa mbele katika kusaidia makundi mbalimbali ya kijamii kipindi hiki cha mwezi wa Ramadhani, na msaada huu ni maalumu kwa kundi la wazee ambalo mara nyingi linasahaulika katika jamii.
Jumuiya ya Wazee Zanzibar (JUWAZA) ilianzishwa mwaka 2013 ikiwa na lengo la kuwaunganisha na kuwasaidia wazee Zanzibar na sasa ina wanachama zaidi ya 1000.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI