MTOTO WA CHINI YA MIEZI SITA HAWATAKIWI KUNYWESHWA MAZIWA YA NG'OMBE-TFNC

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
IMEELEZWA kuwa Mtoto chini ya mwezi hatakiwi kunywa maziwa yeyote isipokuwa ya mama yake, kutokana na maziwa ya ng’ombe  kuwa mazito na hayawezi kumsaidia mtoto katika kukua kwake.

Hayo ameyasema mtaalam wa lishe  wa Taasisi ya Chakula  lishe  nchini (TFNC),Neema Joshua wakati wa semina ya waandishi wa habari ya kuwajengea uwezo wa masuala ya Lishe,amesema maziwa ya ng’ombe wa yanatumika tu pale hakuna namna ya kuweza kupata maziwa mengine.

Amesema watoto chini ya miezi sita wanahitaji maziwa kwa mama na anatakiwa kupewa kila muda katika kuweza kumjenga mtoto kiakili.

Neema amesema katika suala la utapiamlo liko katika viwango vya juu ambapo mwaka 2010 ilikuwa na asilimia 42 hadi sasa imefikia asilimia 34.7 kwa takwimu za mwaka 2014.

Aidha amesema kuwa wale ambao wananyonyesha wakapata mimba akiwa ananyonyesha anaweza  kuuendelea kunyonyesha mtoto na bila kuathiri mimba nyingine.

Amesema wakati akinyonyesha huku ana mimba nyingine anatakiwa karibu na kujifungua miezi miwili aache kwa ajili ya kuupa mwili nguvu kwa mtoto atakayezaliwa na baada ya hapo anaendelea kunyonyesha wote wawili kwa kwanza akifikisha miwili ndipo anaweza kukoma.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI

KOCHA WA AL.AHLY ASEMA YANGA NI TIMU BORA NA NGUMU