SHIRIKA LA HABARI LA MAREKANI INERNEWS LAANDAA MAFUNZO YA SIKU TANO KWA WAANDISHI WA HABARI WA ZANZIBAR JUU YA KURIPOTI UCHAGUZI MKUU.

1
Mkufunzi  na Mwandishi Mkongwe wa Tasnia ya Habari Zanzibar Salim Said Salim akitoa  mada katika mafunzo  ya  siku tano  juu ya kuandika Habari za Uchaguzi Mkuu yaliyoandaliwa na Shirika  la Habari la Marekani  Internews  kwa waandishi wa Habari wa Zanzibar katika Ukumbi wa Umoja wa watu wenye Ulemavu Kikwajuni Mjini Zanzibar.
Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar.
2
Mhadhiri wa Sheria, Kitivo cha Sheria Zanzibar University, Ali Uki akionyesha kitabu cha Sheria cha Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) na kitabu  cha Sheria cha Tanzania na cha Zanzibar  ambavyo  vinawapasa waandishi wa habari kuvisoma na kuzitumia sheria  hizo katika kuandika habari za Uchaguzi Mkuu kwa usahihi.
8
Mwandishi wa Habari wa Gazeti la Zanzibar Leo Hafsa Golo akiwasilisha mada ya grop lake katika mafunzo ya kuandika Habari za Uchaguzi Mkuu yaliyoandaliwa na Shirika la Habari la Ineternews la Marekani katika Ukumbi wa Umoja wa watu wenye ulemavu Kikwajuni Mjini Zanzibar.
5
Afisa Mwandamizi Baraza la Habari Tanzania Ofisi ya Zanzibar Shifaa Said Hassan akiwasilisha mada ya wajibu wa vyombo vya habari katika kuripoti Uchaguzi Mkuu katika mafunzo ya waandishi wa Habari yanayofanyika Ukumbi wa Umoja wa watu wenye ulemavu Kikwajuni Mjini Zanzibar
4 
Baadhi ya waandishi wa habari walioshiriki mafunzo juu ya kuripoti Habari za Uchaguzi kutoka vyombo mbali mbali vya Serikali na binafasi wakifuatilia mada zilizokuwa zikiwakilishwa.
6
Mtayarishaji na Mtangazaji wa vipindi wa Redio Zenj FM Mustapha Mussa akitoa mchango katika mafunzo hayo yanayofanyika Ukumbi wa watu wenye ulemavu Kikwajuni Zanzibar.
7
Washiriki wa mafunzo ya kuripoti Uchaguzi Mkuu wakiwa katika kazi za vikundi wakijadiliana katika kufanikisha mafunzo hayo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.