.Miss Tanzania 2012, Brigite Alfred akizindua ujenzi wa bweni la Albino Buhangija mkoani Shinyanga.
Miss
Tanzania 2012, Brigite Alfred akizungumza wakati wa uzinduzi wa taasisi
yake ya BAF ambayo kwa kushirikiana na Junior Achievement (JA) huku
lengo kuu likiwa ni kutoa elimu ya Ujasiriamali kwa albino Tanzania
nzima. Kushoto ni Kaimu katibu Mkuu wa Jumuiya wa watu wenye ulemavu wa
ngozi (albino), Mohamed Chanzi.
Miss
Tanzania 2012, Brigite Alfred akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya
Albino mara baada ya kuzindua mafunzo ya Ujasiriamali Makumbusho ya
Taifa.
……………
Taasisi
ya Miss Tanzania 2012, Brigitte Alfred Foundation (BAF) kwa
kushirikiana na Taasisi ya Junior Achievement (JA) imeendeleza zoezi la
kutoa mafunzo ya Ujasiriamali kwa wajamii ya watu wenye albino
nchini.Mafunzo hayo ya wiki mbili yalifunguliwa na mkuu wa mkoa wa
Kigoma ambapo jumla ya albino 20 walifaidika na mafunzo hayo
yaliyozinduliwa na mkuu wa mkoa wa Kigoma, kanali mstaafu Issa Machibya.
Mbali ya watu wenye albino, washiriki wengine katika mafunzo hayo
walikuwa wanawake na vijana.
Machibya
alitoa wito kwa taaisis nyingine kuiga mfano taasisi ya Brigitte na
Junior Achievements ambayo mpaka sasa imetoa mafunzo kama hayo kwa
vijana na akina mama 25,000.Mkuu wa mkoa huyo alisema kuwa mafunzo ya
ujasiliamari ni muhimu kwa kila mtu na kupongeza juhudi za mrembo huyo
ambaye mpaka sasa ametoa mafunzo kwa watu wenye albino 70. Kati ya hao
70, albino 50 walipata mafunzo jijini Dar es Salaam.
Comments