TAASISI YA MISS TANZANIA 2012, BRIGITTE ALFRED YATOA MAFUNZO KWA ALBINO 20 KIGOMA

unnamed (69)
.Miss Tanzania 2012, Brigite Alfred akizindua ujenzi wa bweni la Albino Buhangija mkoani Shinyanga.
unnamed (70)
Miss Tanzania 2012, Brigite Alfred akizungumza wakati wa uzinduzi wa taasisi yake ya BAF ambayo kwa kushirikiana na Junior Achievement (JA) huku lengo kuu likiwa ni kutoa elimu ya Ujasiriamali kwa albino Tanzania nzima. Kushoto ni Kaimu katibu Mkuu wa Jumuiya wa watu wenye ulemavu wa ngozi (albino), Mohamed Chanzi.
unnamed (71)
Miss Tanzania 2012, Brigite Alfred akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Albino mara baada ya kuzindua mafunzo ya Ujasiriamali Makumbusho ya Taifa.
……………

Taasisi ya Miss Tanzania 2012, Brigitte Alfred Foundation (BAF) kwa kushirikiana na Taasisi ya Junior Achievement (JA)  imeendeleza zoezi la kutoa mafunzo ya Ujasiriamali kwa wajamii ya watu wenye albino nchini.Mafunzo hayo ya wiki mbili yalifunguliwa na mkuu wa mkoa wa Kigoma ambapo jumla ya albino 20 walifaidika na mafunzo hayo yaliyozinduliwa na mkuu wa mkoa wa Kigoma, kanali mstaafu Issa Machibya. Mbali ya watu wenye albino, washiriki wengine katika mafunzo hayo walikuwa wanawake na vijana.
 
Machibya alitoa wito kwa taaisis nyingine kuiga mfano taasisi ya Brigitte na Junior Achievements ambayo mpaka sasa imetoa mafunzo kama hayo kwa vijana na akina mama 25,000.Mkuu wa mkoa huyo alisema kuwa mafunzo ya ujasiliamari ni muhimu kwa kila mtu na kupongeza juhudi za mrembo huyo ambaye mpaka sasa ametoa mafunzo kwa watu wenye albino 70. Kati ya hao 70, albino 50 walipata mafunzo jijini Dar es Salaam.
 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI