Bi. Samia Othuman Suluhu akipokewa na baadhi ya viongozi na makada wakiwa kwenye mkutano huo. Baadhi ya wananchi wakiwa kwenye mkutano huo.
BAADHI
ya wananchi na wapenzi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wamelazimika
kuuzuia msafara wa mgombea mwenza wa nafasi ya urais leo alipokuwa
njiani akitokea Wilaya ya Same kuelekea Wilayani Mwanga mkoani
Kilimanjaro huku wakimuomba awasalimu na kuzungumza nao, kabla ya
kuendelea na safari yake.
Bi.
Samia Suluhu alilazimika kuusimamisha msafara wake baada ya wananchi
hao kusogea zaidi barabarani wakati akipita huku wakinyoosha mikono ya
kumuomba asimame ili azungumze nao eneo la kilometa chache kabla ya
kuingia njia panda.
Wananchi
hao wengi wakiwa wakinamama walimsimamisha kwa kuingia pembezoni mwa
barabara alipokuwa akipita na hivyo kulazimika kusimama kwa dakika
chache na kuzungumza nao.
Akizungumza
aliwaambia amefarijika na kuwaona na mapenzi makubwa na chama chao
hivyo kuwaeleza kuwa yeye ni mwanamke pia na anajua kwa karibu kero
ambazo wanakabiliana nazo akinamama sehemu mbalimbali na kuahidi endapo
watapata ridhaa pamoja na Dk. John Magufuli atahakikisha anasimamia
vizuri utaratibu wa kuwawezesha akinamama kupitia vikundi vya kijamii
ili waweze kujikwamua kiuchumi pamoja na familia zao.
Comments