Katibu Mkuu Ofisi
ya Makamu wa Rais Sazi Salula akifungua Mkutano wa wadau wa mazingira unaohusu
Miradi ya majaribio nchini wa Mkakati wa Kupunguza Uharibifu wa Misitu
(MKUHUMI) leo jijini Dar es salaam.
Kiongozi wa wawezeshaji
kutoka Asasi isiyo ya kiserikali ya Niras kutoka Finland inayosimamia Miradi ya
majaribio nchini wa Mkakati wa Kupunguza Uharibifu wa Misitu (MKUHUMI) Merja
Makela akitoa mada wakati wa mkutano wa wadau wa mazingira kuhusu namna bora ya
kuhifadhi mazingira na kuboresha usimamizi wa ardhi na kuongeza mapato kutoka
kwenye misitu. Mkutano huo ambao umefanyika leo jijini Dar es salaam
umeandaliwa na Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Serikali ya Norway.
Katibu Mkuu Ofisi
ya Makamu wa Rais Sazi Salula (kushoto) akifuatilia mada wakati wa mkutano wa
wadau wa mazingira kuhusu namna bora ya kuhifadhi mazingira na kuboresha
usimamizi wa ardhi na kuongeza mapato kutoka kwenye misitu. Wa pili kushoto ni
Mkurugenzi wa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Julius Ningu.
Comments