NAIBU KAMISHNA MKUU WA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) NA UJUMBE WAKE WATEMBELEA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

 Uongozi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ukiwa katika kikao na Ujumbe wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) uliotembelea Wizara hiyo.  Wa pili kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, John Mngodo. 
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, John Mngodo akizungumza na ujumbe wa Shrika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) (haupo pichani) uliotembelea Wizara hiyo ambapo masuala mbalimbali kuhusiana na wakimbizi yalijadiliwa.  Tanzania ni mojawapo ya nchi zinazohifadhi wakimbizi, hasa kutoka Ukanda wa Maziwa Makuu.
 Naibu Kamishna Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), Bi. Kelly Clements akizungumza katika kikao na Uongozi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi (haupo pichani) wakati yeye na ujumbe wake walipotembelea Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. Katikati ni Mkurugenzi wa UNHCR, Kanda ya Afrika na kushoto ni Mtendaji Msaidizi wa Naibu Kamishna Mkuu wa UNHCR, Bi. Geraldine Salducci.
Mkurugenzi wa Idara ya Wakimbizi katika Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Harrison Mseke akizungumza katika kikao cha Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na ujumbe wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) wakati ujumbe huo ulipotembelea Wizara. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo.(Picha zote na Abubakari Akida,Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi).
Imeandaliwa na Kitengo Cha  Mawasiliano ya Serikali-Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.