THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone: 255-22-2114512,
2116898
E-mail: press@ikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425
|
|
PRESIDENT’S
OFFICE,
STATE HOUSE,
1 BARACK OBAMA ROAD,
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
|
TAARIFA KWA VYOMBO
VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli amemwapisha Mheshimiwa Majaliwa
Kassim Majaliwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Sherehe za uapisho
zimefanyika leo asubuhi katika Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma na kuhudhuriwa
na viongozi mbalimbali wakiwemo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein, Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar
Balozi Seif Idd, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa
Job Ndugai na Jaji Mkuu wa Tanzania
Mheshimiwa Mohamed Chande Othman
Viongozi wengine
waliohudhuria sherehe hizo ni Jaji Mkuu wa Zanzibar Mheshimiwa Omar Othman
Makungu, Spika wa Baraza la Wawakilishi Mshimiwa Pandu Ameir Kificho, Mawaziri
wakuu wastaafu, Wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama na wabunge.
Mheshimiwa
Majaliwa Kassim Majaliwa ameapishwa kushika wadhifa wa Waziri Mkuu, baada ya
kuteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
na jina lake kupelekwa bungeni ambako wabunge wamelithibitisha kwa asilimia
73.5.
Wakati huo huo,
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo jioni
(Novemba 20, 2015) anatarajiwa kuhutubia na kulizindua Bunge la 11 la Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania katika Ukumbi wa Bunge Mjini Dodoma.
Gerson Msigwa
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
IKULU.
20 Novemba, 2015
Comments