Wachezaji wa DR Congo watuzwa magari ya kifahari

Gari

Image captionKila mchezaji ametunukiwa gari la $60,000
Wachezaji wa timu ya taifa ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wamezawadiwa magari ya kifahari baada ya kushinda Kombe la Taifa Bingwa Afrika kwa wachezaji wa ligi za nyumbani (CHAN).
Rais Joseph Kabila amemtunuku kila mchezaji gari gari la kifahari aina ya Toyota Prado la thamani ya $60,000 (£40,000).
Wachezaji hao pia wamepewa nishani, kwenye hafla iliyoandaliwa ikuluni.
"Asanteni sana kwa ushindi huu. Mmewaunganisha Wakongomani wote," alisema Rais Kabila.
Chui hao wa Kinshasa walitwaa kombe kwa kulaza Mali 3-0 kwenye fainali na kuwa taifa la kwanza kushinda kombe hilo mara mbili.
Mwaka 2009, mara ya kwanza kuandaliwa kwa michuano hiyo, DR Congo waliondoka na ubingwa kwa kulaza Black Stars ya Ghana 2-0 kwenye fainali.
Image copyrightAFP
Image captionDR Congo walilaza Mali 3-0 kwenye fainali
Mwandishi wa BBC Mbelechi Msochi anasema mchezaji Heritier Luvumbu Nzinga aliyeumia kwenye michuano hiyo pia ameahidiwa kwamba atasafirishwa ng'ambo kwa matibabu.
DR Congo
Image captionRais Kabila amewapongeza wachezaji wa timu ya taifa

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI