Rais John Magufuli, ametengua uteuzi wa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Anne Kilango Malecela (pichani).
Akizungumza na Kituo cha Televisheni cha ITV, Rais Magufuli alisema kuwa amemuondoa madarakani Anne Kilango kwa kumdanganya kuwa katika mkoa wake hakuna wafanyakazi hewa.
Imeelezwa kwamba Anne Kilango alitoa taarifa kwa Rais Magufuli kuwa Mkoa huo hakuna wafanyakazi hewa, jambo ambalo limemuudhi rais na kuamua kuchukua hatua hiyo.
Pichani;Mkuu mpya wa mkoa wa Shinyanga Anne Kilango Malecela "Mbula" akiwa ameshikilia mkuki wenye kengele aliposimikwa kuwa Chifu wa Wasukuma katika hafla iliyofanyika wiki iliyopita mkoani humo.
Comments