CDA,UCHUKUZI SC ZAENDELEZA UBABE MEI MOSI


1Mshambuliaji Ramadhani Madebe wa Uchukuzi SC akikokota mpira katikati ya uwanja, huku Mohamed Salum wa GGM akimsogelea. Timu hizo zimetoka satre ya bao 1-1.
7Issack Ibrahim (mwenye mpira) akimtoa Fernand Makanga wa GGM akimzuia asilete madhara. Timu zilitoka sare 1-1.
8Mshambuliaji Oswald Binamungu wa GGM akitafuta mbinu za kumtoka Ally Poloto wa Uchukuzi SC. Timu hizo zilitoshana nguvu kwa kufungana bao 1-1.
3Ramadhani Mwalongo wa Uchukuzi akimalizia mbio za marathoni kwa wanaume na kuibuka mshindi wa tatu kwa kutumia muda wa 0.48:17.
4Ally Zongo wa Uchukuzi SC (kushoto) akiokota karata dhidi ya Kelvin Gadi wa TPDC.
5Mayasa Hamidu (C) wa Uchukuzi SC akiangalia wa kumrushia mpira huku Nathereth Mwanjala (WA) wa Tanesco akisogea kumuwahi . Uchukuzi aliibuka washindi kwa magoli 31-13.
6Prisca Ferdinand wa Uchukuzi SC (kulia) akilamba karata mbele ya mpinzani wake Theodora Stanslaus wa Ujenzi katika mashindano ya Mei Mosi.
…………………………………………………………………………………………….
Na Mwandishi Wetu Dodoma
TIMU za mchezo wa netiboli za CDA Dodoma na Uchukuzi SC jana ziliendeleza ubabe kwa kuwafunga wapinzani wao bila huruma kwenye mashindano ya Mei Mosi yanayoendelea kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.
CDA Dodoma inayoundwa na wachezaji wazoefu iliwafunga TPDC kwa magoli 38-12. Washindi walikwenda mapumziko wakiwa mbele kwa magoli 21-6.
Nao wadada machachari wa Uchukuzi SC wakiongozwa na kocha wao maarufu, Judith Ilunda waliwafunga Tanesco kwa magoli 31-13. Hadi mapumziko washindi walikuwa mbele kwa magoli 19-5.
Wafungaji mahiri wa Uchukuzi SC, Matalena Mhagama alipachika magoli 17 na Grace Mwasote magoli 14, huku Caltace Monampo wa Tanesco alifunga matano na mwenzake Sandra Mfaume magoli nane.
Katika mchezo wa soka, timu ya Uchukuzi SC iliwahenyesha Geita Gold Mine (GGM) na kutoka sare ya bao 1-1. GGM ndio walioanza kupata bao dakika ya 33 kwa mshambuliaji wake Oswald Binamungu aliunganisha krosi ya Quentin George, na Ramadhani Madebe aliyekuwa akihaha uwanja mzima kusaka bao aliisawazishia Uchukuzi katika dakika za nyongeza.
Katika mchezo mwingine wa soka, timu ya Ukaguzi waliwachapa wenyeji CDA kwa magoli 4-1. Victor Ngalawa ndio alikuwa wa kwanza kuandika bao katika dakika ya sita, na Pemsi Msenga alisawazisha katika dakika ya 18.
Ukaguzi waliendelea kuwashambulia CDA na Deo Masanja (mchezaji wa zamani wa Simba SC) aliongeza bao la pili katika dakika ya 33, huku Ally Mpondo alifunga la tatu dakika ya 82 na Yahya Salum alifungala nne dakika ya 89.
Katika mchezo wa riadha mbio za marathoni wanaume ameshinda Atson Mbughuni wa Tamisemi kamaliza kwa 0:35.32, wapili ni Lazaro Lugano wa tanesco katumia 0:42.45 na watatu ni Ramadhani Wakilongo wa Uchukuzi SC katumia 0:48.17.
Upande wa wanawake riadha alishinda Stella Mroso wa TPDC kwa 0:42.36, huku wa pili ni Beltila Genadius wa Tamisemi kwa 0:44.00 na watatu ni Scholastica Halisi wa Uchukuzi kwa 0:49:21.
Katika michezo ya jadi kwa upande wa karata wanawake bingwa ni Sheila Mwihava wa Tanesco alimshinda Mayasa Kambi wa UDOM katika fainali na mshindi wa tatu ni Bupe Munisi wa Mawasiliano, kwa upande wa wanaume ametwaa ubingwa Haji Chilo wa UDOM, huku wa pili ni Omari Said wa Tanesco na watatu ni Ally Zongo wa Uchukuzi SC

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA