MATUKIO ZAIDI ZIARA YA RAIS WA SUDANI KUSINI SALVA KIIR AWASILI NCHINI NA KUTIA SAINI MKATABA WA KUJIUNGA RASMI NA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI
Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir Mayardit akiwa amesimama na Mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakati wimbo wa Taifa ukipigwa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir Mayardit wakipiga makofi mara baada ya kufurahishwa na wimbo wa bendi ya Polisi iliyokuwa ikitumbuiza Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir Mayardit kabla ya utiaji saini wa Mkataba wa Sudani Kusini kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki ikulu jijini Dar es Salaam.
Comments