Mkurugenzi
wa manispaa ya Ilala Isaya Mgulumi (mwenye miwani) akiwaeleza mawaziri
wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy
Mwalimu (katikati) na Waziri wa Kilimo na Mifugo, Mwigulu Nchemba
(kushoto) akiwaelezea hali ya ukarabati wa machinjio hayo.
Waziri
wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Mh. Mwigulu Nchemba kwa pamoja na Waziri wa
Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu
wametembelea machinjio ya Vingunguti na kuona jinsi hali ilivyo katika
eneo hilo.
Pamoja
na kutembelea eneo hilo ambalo lilikuwa limefungiwa kuchinja nyama,
mawaziri hao wameruhusu kwa siku tatu kuchinja huku wakitoa maagizo kwa
Halmshauri ya Manispaa ya Ilala kuhakikisha wanapafanyia marekebisho.
Mkaguzi
toka TFDA Dkt. Mwanga Itikija (mwenye shati la pink) akiwaonesha
mawaziri hao eneo ambalo lilikua likiuzia nyama kwa reja reja kinyume na
kanuni ya afya.
Baadhi ya wafanyabiashara wa machinjio hayo wakifuatilia ziara hiyo.
Mbunge
wa jimbo la Segerea, Bona Kalua, akiongea na wanachama wa Umoja wa
Wafanyabiashara wa Ng'ombe na mazao yake (UWAMI) kwenye mkutano wa
pamoja na mawaziri hao.
Waziri
Ummy Mwalimu akiongea na Wanachama wa umoja huo, ambapo aliwasisitiza
kufanya biashara kwa kuzingatia kanuni za afya na kumlinda mlaji hivyo
kuwa makini na utunzaji wa mazingira pamoja na mazao wanayoyauza
machinjioni hapo.
Waziri
Mwigulu Nchemba akiongea na Umoja huo na kuwapatia siku tatu ili
waendelee na uchinjaji wa ng'ombe walizonazo na baada ya hapo
wataendelea na ukarabati wakati huo machinjio ya mazizini yatakua
yamekamilisha ukarabati na kufunguliwa.
Comments