Siku ya
Jumamosi (16/04) Jumuiya ya Watanzania waishio katika jiji la Houston na
miji mingine ya karibu ilifanya Ibada Takatifu katika kanisa la Umoja
kumuaga mpendwa wao Henry Kiherile aliyefariki wiki moja na nusu
iliyopita baada ya kupigwa risasi na watu wasiojulikana.
Ibada
hiyo ilihudhuriwa na idadi kubwa ya watu waliokuwa na huzuni kubwa juu
ya kifo hicho kilichogusa mioyo ya watu wengi. Mwili wa marehemu Henry
unatarajiwa kusafirishwa jioni ya leo kuelekea nyumbani Tanzania kwa
mazishi yanayotarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam siku ya Ijumaa
tarehe 22/04/2016. Pata picha za Misa hiyo hapa chini.
Marehemu Henry Kiherile enzi za uhai wake
Mr.& Mrs. Tenende ( Baba na Mama mkubwa wa marehemu ) wakiwa kanisani
Waombolezaji
Gari lililobeba mwili wa Henry likiingia kanisani
Comments