JAMHURI
YA MUUNGANO WA TANZANIA
KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU
Simu:
255-22-2114512, 2116898
E-mail: press@ikulu.go.tz
Faksi: 255-22-2113425
|
OFISI YA RAIS,
IKULU,
1 BARABARA YA BARACK
OBAMA,
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
|
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais
wa Jamhuri ya Burundi Mheshimiwa Pierre Nkurunziza amemtumia ujumbe Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ambaye pia ni
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, akimhakikishia kuwa hali ya Burundi
ni shwari na amemuomba awasihi wananchi wa Burundi waliokimbia nchi yao warejee
nyumbani.
Barua
yenye ujumbe huo, imewasilishwa kwa Rais Magufuli leo tarehe 16 Aprili, 2016
Ikulu Jijini Dar es salaam na Mjumbe Maalum wa Rais Nkurunziza ambaye ni
Mnadhimu wa Jeshi la Burundi Meja Jenerali Evariste Ndayishimiye.
Meja
Jenerali Ndayishimiye amemueleza Rais Magufuli kuwa Rais wa Burundi Mheshimiwa
Pierre Nkurunziza amemtuma kuleta barua hiyo pamoja na shukrani za dhati kwa
Tanzania ambayo ni rafiki, jirani na ndugu wa kweli wa Burundi kwa ushirikiano
mzuri inaoupata kutoka Tanzania katika masuala mbalimbali.
"Burundi
na Tanzania ni ndugu wa kweli, na sisi Burundi tunaiona Tanzania na nchi yetu
kama Baba na mtoto wake" amesema
Meja Jenerali Ndayishimiye.
Kwa
upande wake Rais Dkt. John Pombe Magufuli amemshukuru Rais Nkurunziza kwa
kumtumia ujumbe huo na amemhakikishia kuwa Tanzania itaendelea kuwa rafiki na
ndugu wa dhati wa Burundi kama ambavyo mahusiano ya nchi hizi mbili yamejengwa
tangu zamani.
Kuhusu
hali ya Burundi Rais Magufuli amesema anaamini kuwa wasuluhishi mgogoro wa nchi
hiyo ambao ni Rais wa Jamhuri ya Uganda Mheshimiwa Yoweri Kaguta Museveni na
Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu wa Tanzania Mheshimiwa Benjamin William Mkapa
watafanikiwa kusuluhisha mgogoro huo.
"Naomba
umwambie Rais Mheshimiwa Nkurunziza kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana na
Burundi, na tunawaombea mgogoro uishe ili muendelee kuijenga nchi yenu"
Amesema Rais Magufuli.
Gerson
Msigwa
Kaimu
Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar
es salaam
1
Comments