JAMHURI
YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA
YA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
MHE. DKT. JOHN JOSEPH POMBE MAGUFULI KUWEKA JIWE LA MSINGI LA UJENZI WA
BARABARA YA JUU (FLYOVER) YA TAZARA NA KUFUNGUA DARAJA LA KIGAMBONI JIJINI DARA
ES SALAAM
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
inapenda kutaarifu Umma kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt.
John Pombe Joseph Magufuli, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika sherehe za
uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa barabara ya juu (Flyover) katika makutano ya TAZARA na ufunguzi wa Daraja la Kigamboni
jijini Dar es Salaam.
Siku ya Jumamosi tarehe 16 Aprili, 2016
Mheshimiwa Rais ataweka jiwe na msingi la ujenzi wa barabara ya juu katika
makutano ya barabara Nyerere na Mandela (Flyover
ya TAZARA).
Jumanne tarehe 19 Aprili, 2016
Mheshimiwa Rais atafungua rasmi Daraja la Kigamboni lenye urefu wa mita 680 na
barabara unganishi (approach roads)
upande wa Kurasini na Kigamboni zenye urefu wa kilometa 2.5. Ujenzi huu umefanywa na Kampuni ya China
Railway 15 Group ilishirikiana na Kampuni ya China Bridge Engineering Group.
Aidha wakati tunasubiri uzinduzi rasmi,
Wananchi na magari yenye uzito usiozidi tani 10 yataruhusiwa kutumia Daraja la Kigamboni
kuanzia Jumamosi tarehe 16 Aprili, 2016 ili kuwawezesha kuelewa vizuri
miundombinu na matumizi ya daraja.
Utekelezaji wa miradi hii ni mojawapo ya
jitihada za Serikali za kuboresha miundomninu na kupunguza msongamano wa magari
katika jiji la Dar es salaam.
Imetolewa na;
Eng. Joseph M. Nyamhanga
Katibu Mkuu (Ujenzi)
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na
Mawasiliano
14 Aprili, 2016
Comments