UJUMBE WA MAWAZIRI NA WAFANYABIASHARA WA CZECH REPUBLIC WAFANYA KONGAMANO LA UWEKEZAJI DAR.

2
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo na Misitu  wa Serikali ya Czech Republic Bw. Dusan Benza akizungumza katika kongamano la wafanyabiashara wa nchi hiyo na watanzania lililofanyika leo kwenye hoteli ya New Africa jijini Dar es salaam.
Mawaziri wawili Kilimo na Viwanda wa Jamhuri ya Jamhuri ya Czech  wakiongozana na wafanyabiashara zaidi ya thelathini wako nchini kwa ajili ya kutafuta na kujionea fursa za uwekezaji  nchini Tanzaniam  Mkutano huo umeandaliwa kwa pamoja na Tanzania Investiment Bank (TIB), Ubalozi wa Szech Republic nchini Kenya na Tanzania House Of Business Company Limited (THB).
Ujumbe huo metembelea wizara ya Kilimo na wizara ya Viwanda na Biashara  na kusaini mikataba ya ushirikiano wa kibiashara na uwekezaji hapa nchini na nchi ya Szech Republic ili kuunganisha masuala ya kibiasha na uwekezaji na kuwezesha wafanyabiashara wa nchi hizi kuwekeza katika masuala ya biashara, Teknolojia  na Kilimo kwa ujumla.(PICHA NA JOHN BUKUKU-FULLSHANGWE-DAR ES SALAAM)
3
Balozi wa Heshima na Mwakilishi wa Ubalozi wa Czech Republic hapa nchini  John Chaggama  akizungumza na mmoja wa viongozi wa ujumbe huo huku   Marian Jureck Waziri wa Kilimo wa Czech akisikiliz kwa makini.
4
Injinia Michal Basovnik  wa kampuni ya Impuls  akitoa mada kuhusu shughuli mbalimbali zinazotolewa na kampuni yao ambayo ina tawi pia nchini Zambia.
57
Injinia Martin Adamuska  wa kampuni ya NWT kutoka nchini Czech Republic akifafanua jambo wakati alipokuwa akielezea mambo mbalimbali yanayofanya na kampuni yao lakini pia fursa mbalimbali zinazoweza kuwekezwa.
8
Injinia Petr Pawlica wa wa kampuni ya PAWLICA pia ametoa mada katika kongamano hilo na kuelezea teknolojia ya kampuni hiyo katika masuala ya Kilimo.
9
Bw. Godffrey Kirenga wa SAGCOT CENTER LIMITED akiwaelezea wafanya biashara hao juu ya fursa mbalimbali zilizopo hapa nchini katika uwekezaji wa kilimo.
10
 Mkurugenzi mtendaji Mkuu wa Tanzania Private Sector Foundation(TPSF) Godfrey Simbeye akizungumza katika kongamano hilo kulia ni  John Chaggama Balozi wa Heshima na Mwakilishi wa Ubalozi wa Czech Republic nchini Tanzania.
1112
Kutoka kulia ni Mr Charles Chandika Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Tanzania House Of Business Company Limited, Pan Arnold  Mturi Charge de Affairs at the Szech Consolate  nchini Tanzania, Elipina Makungu na Bahija Salim wakijadiliana jambo wakati wa kongamano hilo la wafanya biashara.
13
Mkurugenzi mtendaji Mkuu wa Tanzania Private Sector Foundation(TPSF) Godfrey Simbeye akizungumza na Pan Arnold  Mturi Charge de Affairs at the Szech Consolate  nchini Tanzania  wakimsikiliza mmoja wa maofisa kutoka wizara ya mambo ya nje wakati akizungumza nao.
14
Mkurugenzi mtendaji Mkuu wa Tanzania Private Sector Foundation(TPSF) Godfrey Simbeye na  John Chaggama Balozi wa Heshima na Mwakilishi wa Ubalozi wa Czech Republic nchini Tanzania wakizungumza na Injinia Vladmir Pikora wa benki  ya Czech Export Bank mara baada ya nusu ya kwanza ya majadiliano kati ya wafanya biashara wa Tanzania na Szech Republic katika kongamano lililofanyika kwenye hoteli ya New Africa jijini Dar es salaam.
15
 John Chaggama Balozi wa Heshima na  Mwakilishi wa Ubalozi wa Czech Republic nchini Tanzania akifafanua jambo kwa waandishi wa habari kuhusu ujio wa wafanyabiashara hao.
16
Mkurugenzi mtendaji Mkuu wa Tanzania Private Sector Foundation(TPSF) Godfrey Simbeye akizungumza na waandishi wa habari juu ya umuhimu wa ujio wa wafanyabiashara hao na kongamano hilo kwa wafanyabiashara wa Tanzania ya Czech Republic katika masuala mazima ya kibiashara na uwekezaji.
17
Baadhi ya wafanyabiashara kutoka nchini Czech Republic wakiwa katika kongamano hilo lililofanyika kwenye hoteli ya New Africa jijini Dar es salaam
1819
Baadhi ya wafanyabiashara wa Tanzania wakihudhuria kongamano hilo.
20
Baadhi ya waalikwa kutoka taasisi mbalimbali za Tanzania masuala ya biashara na uwekezaji wakiwa katika kongamano hilo.
21
 John Chaggama Balozi wa Heshima na Mwakilishi wa Ubalozi wa Czech Republic nchini Tanzania akimsikiliza Pan Arnold  Mturi Charge de Affairs at the Szech Consolate  nchini Tanzania.
22
Elipina Makungu na Bahija Salim wakifurahia  jambo wakati wa kongamano hilo la wafanyabiashara wa Czech Republic na Tanzania kwenye hoteli ya New Africa jijini Dar es salaam.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.