WATOA MSAADA WA MILIONI 1.7 KUJENGA CHOO CHA WALIMU


Mazingira na hali halisi ya Choo cha Walimu

Choo cha Wanafunzi ni bora na cha kisasa tofauti na choo cha Walimu


 
Diwani wa Kata ya Isapulano Wilaya ya Makete Alphonce Mbilinyi akizungumza neno baada ya kupokea msaada wa fedha wa ajili ya ujenzi wa Choo cha Walimu katika Shule ya Msingi Ivilikinge.

Afisa Mtendaji akipokea Msaada kutoka kwa kiongozi wa Mwapima Forum ndugu Tito Tweve

Baadhi ya viongozi wa Mwapima forum wakikabidhi mfuko wa saruji kwa viongozi wa Kijiji na Kamati ya Shule ya Ivilikinge kwa ajili ya ujenzi wa Choo cha Walimu


Mwalimu Mkuu shule ya Msingi Ivilikinge, Ibrahim Fungo, akipokea kipande cha Malumalu kwa ajili ya kujengea Choo cha Walimu shuleni kwake

Mwalimu Mkuu akipokea Peni kwa ajili ya matumizi ya walimu

Baadhi ya viongozi wakikabidhiana vifaa mbali mbali kwa ajili ya ujenzi wa Choo cha Walimu

Tito Tweve akizungumza na wananchi wa Ivilikinge kuhusu kuguswa na hatimaye kutoa msaada wa vifaa vya ujenzi wa Choo cha Walimu

Wanachama wa Mwapima forum wakiangalia mazingira ya Choo cha walimu wa Shule ya Msingi Ivilikinge ambacho kimechakaa na hakifai kwa matumizi ya binadamu

Wanafunzi wakitoa burudani




VIJANA nchini wameshauriwa kuwa na utamaduni wa kukumbuka asili yao kwa kurudi kushiriki katika shughuli za maendeleo katika maeneo waliyotoka badala ya kuwaachia wazazi pekee licha ya umri wao kuwa mkubwa.

Wito huo ulitolewa na Baadhi ya Vijana waishio nje ya Kijiji cha Ivilikinge Kata ya Isapulano Wilaya ya Makete mkoani Njombe waliounda umoja wao unaojulikana kwa jina la Mwapima Forum wakati wa hafla ya kukabidhi msaada wa vifaa vya ujenzi wa vyoo vya walimu katika Shule ya Msingi Ivilikinge.

Akisoma taarifa kwa niaba ya wenzake, Mratibu wa Mwapima Forum, Award Mpandila alisema umekuwa utamaduni kwa vijana kutoka katika maeneo waliyozaliwa na kukulia na kuelekea sehemu nyingine kutafuta maisha lakini pindi wanapofanikiwa hujisahau na kushindwa kurudi kuchangia shughuli za maendeleo.

Alisema kutokana na hali hiyo baadhi ya Vijana wapatao 60 waliosoma shule ya Msingi Ivilikinge kutoka maeneo mbali mbali ya Ndani na Nje ya Nchi walijikusanya kupitia mitandao ya kijamii kwa lengo la kufahamiana na kupeana taarifa za kijijini kwao kuona kama kuna changamoto ambazo wanaweza kusaidia kuzitatua.

Mpandila alisema umoja huo ambao ulianzishwa Disemba 21, mwaka jana baadhi ya wanachama wake walibaini kuwepo kwa Changamoto ya Choo cha Walimu katika Shule hiyo huku Wanafunzi wakitumia vyoo vya kisasa vilivyojengwa kwa msaada wa watu wa Marekani(USAID).

Alisema umoja huo uliamua kuchangishana ili kutatua tatizo la Choo kwani Walimu walikuwa wakitumia Choo kilichochakaa na wakati mwingine walilazimika kufuata huduma hiyo majumbani mwao.

Alisema katika makusanyo hayo zaidi ya shilingi Milioni 1,763,700 zilikusanywa ambazo zitaweza kumudu gharama za ujenzi wa Choo kimoja chenye matundu mawili hadi kukamilika kutokana na mahitaji muhimu kununuliwa na kukabidhi kwa serikali ya Kijiji na Kamati ya Shule kwa ajili ya usimamizi.

Akisoma risala ya Shule katika hafla hiyo, Mwalimu Atuwene Fungo alisema Walimu walikuwa wakitumia kwa hofu kubwa choo chao kutokana na kuchakaa kwani kilijengwa muda mrefu bila kuwa na miundombinu ya kudumu ambapo kilijengwa Mwaka 1976 wakati shule hiyo ikianzishwa.

Alisema msaada uliotolewa na vijana hao utasaidia Walimu kuokoa muda wa kufuata huduma ya choo mbali na mazingira ya shule hivyo itarahisha wao katika ufundishaji kutokana na mwalimu kuwepo muda wa kutosha katika mazingira ya shule.

Alisema changamoto zingine ni upungufu wa Walimu, uchakavu wa miundombinu, madawati, upungufu wa Walimu na vifaa vya kufundishia jambo ambalo Vijana waishio nje ya Kijiji hicho waliahidi kutatua baadhi kama Madawati na vifaa vya kufundishia pamoja na ujenziwa madarasa mapya.

Kwa Upande wake Diwani wa Kata ya Isapulano ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo, Alphonce Mbilinyi, licha ya kuwapongeza vijana hao kwa juhudi walizoonesha za kukumbuka nyumbani kwao kwa kuwasaidia walimu aliahidi kusimamia ujenzi wa Choo hicho na kuhakikisha kinakamilika ndani ya siku kumi na nne.

“Sina maneno mengi ya kuongea nimeguswa na jambo la hawa vijana nawapongeza sana ni mfano wa kuigwa na watu wengine mkumbuke kuja kutusaidia wazee wenu, nawaahidi ujenzi wa hiki choo utaanza haraka sana na ndani ya wiki mbili utakuwa umekamilika, Hapa kazi tu” alisema Diwani Mbilinyi.

Nao baadhi ya Wakazi wa Kijiji cha Ivilikinge, Emelite Sanga,Luthi Msigwa,Ezron Tweve na Cosmas Luvanda walisema wanafarijika kuona watoto wao wanakumbuka nyumbani na kusaidia shughuli za maendeleo leo kwa jambo hilo litawapunguzia mlundikano wa michango mbali mbali katika Kijiji chao.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA