HABARI KUTOKA TELEVISHENI

Watu watatu waumini wa dini ya kiislamu wameua kwa kukatwakatwa mapanga na shoka wakakti walipokuwa wakiswali katika msikiti wa Utemini mkoani Mwanza. https://youtu.be/mPHIYC88WsE
Wizara ya mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika mashariki imetoa wito kwa taasisi za serikali kuhakikisha kuwa wanatumia alama za jumuiya ya Afrika mashariki ambazo ni bendera ya jumuiya na wimbo wa jumuiya.https://youtu.be/MhwAr_s6ShQ

Kuongezeka kwa migogoro kati ya wafugaji na wakulima katika wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro kumeelezwa kuchangiwa na viongozi wa mitaa na vijiji kwa kufanya mogogoro hiyo kuwa mtaji. https://youtu.be/76BJhRFpnAM

Mamlaka ya chakula na dawa nchini TFDA imefanya ukaguzi wa maerekebisho yaliyokua yakifanyika katika machinjio ya Vingunguti na kusema kuwa bado marekebisho hayo hayaridhishi. https://youtu.be/IOPsx2Di1Ew

Wasamaria wema wameombwa kumsaidia mtoto Ahmed Thabiti mwenye mwenye umri wa miaka miwili na nusu ambapo anasumbuliwa na tatizo la kusinyaa kwa ubongo na matibabu yake yanahitaji kiasi cha shilingi milioni 99.https://youtu.be/zFqIacuncTM

Hali ya upatikanaji wa samaki katika soko la Feri jijini Dar es salaam imeendelea kuwa duni ambapo imesemekana ukosefu wa vitendea kazi na hali ya hewa ndio visababishi vikuu vya tatizo hilo. https://youtu.be/2fy9uQ2scoQ

Wafanya biashara wa soko kuu la mjini Geita katika wilaya ya Geita wameiomba serikali kuwachimbia kisima cha maji na kuwajengea vyoo katika soko hilo ambapo ndizo changamoto kuu za miundombinu zinazokwamisha biashara zao sokoni hapo. https://youtu.be/46dF05XfGJk

Wafanyabiashara wa vinywaji na vyakula ikiwemo mamalishe na wamiliki wa baa na nyumba za kulala wageni wametakiwa kuzingatia kanuni za afya ili kuepusha magonjwa yanayosambaa kwa kasi katika maeneo hayo.https://youtu.be/3Rqn-mTz87U

Timu ya Serengeti boys imefanikiwa kutoa sare ya mbili kwa mbili dhidi ya timu ya vijana ya Korea na kufanya kufikisha alama tano. https://youtu.be/yKAFPdg9eK4

Baada ya timu ya Yanga kufanikiwa kutinga hatua ya makundi katika michuano ya kombe la shirikisho uongozi umelalamikia waamuzi waliochezesha mchezo wao dhidi ya esperanse huko Angola kuwa hawakutenda haki hivyo watawashitaki kwa shirikisho la soka Afrika. https://youtu.be/07L4x9ozXhM

Bondia Kosmas Cheka anatarajia kupanda ulingoni kupambana na bondia kutoa nchini Malawi wakiwania mkanda wa UBO kwa pambano la roundi kumi na mbili. https://youtu.be/e2vOA6_yO7M

Bendi ya muziki ya Twanga Pepeta inatarajia kuzindua albamu yake ya kumi na tatu katika  mkoa wa Mwanza ambapo wanategemea kuizindulia katika hoteli ya Villa Park. https://youtu.be/oL-MaxsWQiA

Mkazi wa Mburahati jijini Dar es Salaam amejishindia pikipiki kwenye mchezo wa bahati na sibu unaoendeshwa na kampuni ya Global Publishers. https://youtu.be/gWkCHTC6esY

Bingwa mtetezi wa kikapu nchini Marekani Golden state  jana wamelipa kisasi kwa wenzao Oklahoma thunders kwenye michuano ya kuwania kuingia fainali za kanda. https://youtu.be/NE_ir7BPyPk

Watu 15 waliokuwa wameficha sura zao wamewaua watu 3 kwa kuwapiga mapanga na mashoka wakiwa msikitini mkoani mwanza; https://youtu.be/YTnaHoib4yU
Mkuu wa mkoa wa Tanga Martin Shigela amewatoa hofu wananchi na wakazi wa mkoa huo kwa kuwaambia kuwa hali ya usalama mkoani humo imeimarishwa kila kona; https://youtu.be/pqfuBFwsTmk
Kamanda wa polisi mkoani Mara anawashikilia watu wawili kwa tuhuma za kusafirisha madawa ya kulevya aina ya Mirungi zaidi ya magunia 15 wakielekea mkoani Mwanza; https://youtu.be/FeaulK7iMuw
Rais Dkt Magufuli amesema Tanzania iko mbioni kuanza ujenzi wa kiwanda kikubwa cha mbolea wilayani Kilwa mkoani Lindi; https://youtu.be/9NpO0mzPghg
Watu wasiojulikana mkoani Mbeya wamevamia barabara kuu ya kutoka mjini Mbeya mpaka Chunya na kuiba vyuma vya alama za barabarani; https://youtu.be/x89uRqiu9Uk

Serikali imeongeza fedha kwa asilimia 50 kwa wakala wa umeme vijijini REA ili kuhakikisha vijiji vingi vinapatiwa umeme nchini; https://youtu.be/DiJcrq9gvk4   

Kampuni ya Trademark East Africa wamesema watatoa zawadi kwa wajisiliamali wabunifu watakaofanikiwa kubuni mradi mzuri wa usafirishaji; https://youtu.be/5RMSET580Vs
Wakazi wa Longido mkoani Arusha waiomba serikali kupitia TASAF kuwapatia mbegu bora za mifugo badala ya fedha ambazo wanashindwa kuzitumia vizuri; https://youtu.be/800QX3eozBs

Watanzania wametakiwa kulinda na kuenzi utamaduni wao ili kuwawezesha na kuheshimika duniani kama taifa huru lenye tmila na tamaduni zake; https://youtu.be/nLwhzmXoQ3k  

Timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 Serengeti boys imetinga hatua ya nusu fainali baada ya leo kutoka sare ya mabao 2 kwa 2 na Korea kusini huko nchini India; https://youtu.be/lXZgji6ID5Q

Attachments area
Preview YouTube video Mauwaji Ya Kikatili Kwa Waumini Msikitini Preview YouTube video Wizara Yasisitiza Utumiaji Wa Alama Za Jumuiya Ya EAC Preview YouTube video Wakulima Kumaliza Migogoro Wenyewe Mvomero Preview YouTube video TFDA Yaendelea Kupigilia Msumari Machinjio Ya Vingunguti Preview YouTube video Mtoto Mgonjwa Aombewa Msaada Wa Matibabu Preview YouTube video Samaki Waadimika Jijini Dar es Salaam Preview YouTube video Soko Kuu La Geita Lakosa Maji Na Vyoo Preview YouTube video Wafanyabiashara Wa Vyakula Na Vinywaji Waaswa Kuhusu Usafi Preview YouTube video Serengeti Boys Yaendeleza Ubabe Huko India Preview YouTube video Yanga Kumshitaki Mwamuzi Preview YouTube video Cheka Kupambana Na Bondia Kutoka Malawi Preview YouTube video Twanga Pepeta Kuzindua Albamu Yao Mwanza Preview YouTube video Apata Pikipiki Kwenye Bahati Na Sibu Preview YouTube video Golden State Walipa Kisasi Preview YouTube video Watu Watatu Wauawa Kikatili Mkoani Mwanza wakiwa Msikitini Preview YouTube video Hali ya Usalama Tanga Yaimarishwa new Preview YouTube video Watu Wawili Matatani kwa Usafirishaji Mirungi Preview YouTube video Serikali Kuanza Ujenzi Kiwanda cha Mbolea Mkoani Lindi new Preview YouTube video Mbeya Waharibu Barabara Zao Wenyewe new Preview YouTube video Wakala wa Umeme Vijijini REA Aongezewa Bajeti Preview YouTube video Trademark Watangaza Ajira kwa Vijana Wabunifu Preview YouTube video Longido Waiomba TASAF Mifugo Bora new Preview YouTube video Watanzania Washauriwa Kuenzi Utamaduni Wao Preview YouTube video Serengeti Boys Yatinga Nusu Fainali Huko India new

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.