HABARI KUTOKA VITUO VYA TELEVISHENI

SIMU.TV: Makamu wa rais Mama Samia Suluhu amelaani mauaji yaliyotokea jana katika kijiji cha Sima wilayani Sengerema mkoani Mwanza baada ya watu wasiojulikana kuvamia familia moja na kuua watu wa saba;https://youtu.be/bLmNhjMqfHY

SIMU.TV: Wananchi wilayani Tandahimba mkoani Mtwara waiomba serikali kupeleka sukari baada ya bidhaa hiyo kukosekana kabisa; https://youtu.be/QjQ4VLOuwR4
SIMU.TV: Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda aapishwa rasmi leo nchini tayari kwa kutumia muhula mwingine wa uongozi kama rais; https://youtu.be/Tn2yglavPu0

SIMU.TV: Serikali imefanya mabadiliko katika kanuni za uvunaji wa misitu ili kuruhusu wananchi wanaozunguka eneo husika kufaidika na misitu yao; https://youtu.be/LRUruQKVJMA

SIMU.TV: Wauguzi mkoani Tabora wameadhimisha siku ya wauguzi duniani kwa kuelezea changamoto mbalimbali zinazowakumba katika utendaji kazi wao; https://youtu.be/SlJFQTKs2g4

SIMU.TV: Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda amewataka wauguzi nchini kufanya kazi zao kwa kuzingatia taratibu na weledi kwa kazi zao ikiwa ni pamoja na kuepuka lugha chafu kwa wagonjwa; https://youtu.be/dp50zpVfN4s

SIMU.TV: Mamlaka ya maji safi na majitaka jijini Dar es salaam DAWASCO wamemkamata meneja wa hotel ya Marriot jijini Dar es salaam kwa tuhuma za kujiunganishia maji kinyume cha sheria; https://youtu.be/9hD5UkXEbqg

SIMU.TV: Shirika la maendeleo ya petroli nchini TPDC lajipanga kutumia zaidi ya bil.40 za kitanzania kujenga kiwanda cha kuchakata gesi asilia mkoani Lindi; https://youtu.be/w_STuFrmW0g

SIMU.TV: Benki ya maendeleo ya kilimo nchini TADB imetoa zaidi ya shilingi bil.2 kwa wakulima wajasiliamali nchini huku pia ikijipanga kutoa zaidi ya shilingi 40 kuendeleza sekta ya kilimo; https://youtu.be/Zo_JXum5fDU

SIMU.TV: Makampuni ya utalii nchini yameiomba serikali kuitengea bodi ya utalii ili kuwezesha kuvitangaza vyanzo vyetu vya utalii kimataifa zaidi; https://youtu.be/-QGg6quwv4c

SIMU.TV: Mchezo wa bahati nasibu wa taifa unatarajia kuanza kutimua vumbi nchini may 24 katika vituo zaidi ya elfu 20 nchi nzima; https://youtu.be/Qr5wL_LMftE

SIMU.TV: Shirikisho la soka nchini TFF limeombwa kuingilia kati sakata linaloendelea katika timu ya Stand United wanaovutana kuhusu kubadilishwa kwa timu kujiendesha kikampuni; https://youtu.be/kyepxxEkezg

SIMU.TV: Zaidi ya wachezaji 80 wa mchezo wa golf wamejiandikisha katika mashindano ya mchezo huo;https://youtu.be/CisYZEbMyHA

SIMU.TV: Shirikisho la wasanii Tanzania SHIWATA limepanga kumkabidhi hekari 5 mshambuliaji wa wa kimataifa Mbwana Samatta huko Mkuranga; https://youtu.be/60WDbJiRP-k

SIMU.TV: Wanafunzi wa chuo cha ustawi wa jamii wafanya michezo mbalimbali chuoni kwao hapo ikiwa ni kuadhimisha kwa siku ya chuo hicho; https://youtu.be/n70bExM1Jho

SIMU.TV: CAF Yatangaza mabadiliko ligi ya mabingwa na shirikisho Afrika kwa kuongeza makundi manne badala ya mawili ya hapo awali; https://youtu.be/_z9OCmoV8oA

SIMU.TV: Kamati ya ulinzi ya mkoa wa Dar es Salaam imeendelea kukagua maghala ya wafanyabiashara wanaodaiwa kuficha sukari ambapo leo wamebaini zaidi ya tani elfu tano kwenye ghala la Mohamedi Enterprise.https://youtu.be/wqAdsaIOiWA  

SIMU.TV: Zoezi la kukamata sukari limeendelea Dar es Salaam ambapo mfanyabiashara mmoja maeneo ya Manzese amekutwa na mifuko zaidi ya mia ya sukari bila kuwa na kibali cha kuhifadhi bidhaa hiyo. https://youtu.be/f2DAevNGhAo

SIMU.TV: Wananchi wa wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma wamelalamikia upandaji wa bei ya bidhaa za sukari na mafuta ya kupikia na kuwafanya kutomudu kununua bidhaa hizo. https://youtu.be/QNiIWhtU01A  

SIMU.TV: Makamu wa rais Bi Samia Suluhu Hassani amewataka viongozi na wanasiasa kufuata utaratibu wa kiutumishi wakati wa kuwasimamisha kazi wauguzi na wafanyakazi wengine. https://youtu.be/dZS1H5b31_c

SIMU.TV: Serikali ya Tanzania mpaka sasa haina sheria ya majenzi yaani building act hali inayosababisha kukosekana kwa hatua sahihi za kufuatilia pale jengo linapojengwa chini ya kiwango. https://youtu.be/7BiBF3Krbfs

SIMU.TV: Wananchi wa jiji la Dar es Salaam wameonekana kuelewa jinsi ya kutumia mabasi ya mwendo kasi ikiwa ni pamoja na matumizi ya kadi za kulipia. https://youtu.be/i48dJgh6P9Y

SIMU.TV: Serikali imekutana na wawekezaji wakubwa na makampuni yanayojihusisha na uwekezaji wa gesi ili kuhakikisha bidhaa hiyo inazalishwa kwa kiwango cha kuweza kuuzwa nje ya nchi. https://youtu.be/UMRMGsAFYt4

SIMU.TV: Wakulima wa korosho mkoani Mtwara wameupongeza mfuko wa kuendeleza uzalishaji wa zao la korosho kwa kutekeleza zoezi la ugawaji wa pembejeo kwa wakati. https://youtu.be/MIHt4oRgi9I

SIMU.TV: Wafanyabiashara wadogo wa zao la mpunga kutoka soko la Sido mkoani Mbeya wamelalamikia gharama za mizani tozo za ushuru na kutopata elimu kutoka kwa wakala wa vipimo nchini kuwa ni changangamoto kwenye biashara yao. https://youtu.be/FuvNY64niiY  

SIMU.TV: Uongozi wa klabu ya Yanga umetoa pongezi kwa wachezaji wa klabu hiyo kwa kujituma na kuwezesha kuchukua kombe la ligi kuu Tanzania bara kwa mara ya pili mfululizo. https://youtu.be/GySVXychRmo

SIMU.TV: Michuano ya Lugalo gofu inatarajiwa kufanyika kwa siku mbili jijini Dar es Salaam ambayo itachezwa jumamosi na jumapili wiki hii. https://youtu.be/imSG9McnVZU   

SIMU.TV: Bodi ya michezo ya kubahatisha nchini imewataka wananchi wanaoshiriki michezo hiyo kusoma na kuelewa haki zao na namna wanavyotakiwa kulipwa zawadi zao wanaposhinda. https://youtu.be/lHqcUXe2GuA

SIMU.TV: Imeelezwa kuwa licha ya mchezo wa bao kutopewa kipaumbele nchini mchezo huo umekua na mchango mkubwa kwa wanafunzi mashuleni hususan somo la hesabu. https://youtu.be/JOmeTWeR6c0  

SIMU.TV: Aston Villa New Castle United na Norwich city zimeshuka daraja katika ligi kuu ya Uingereza ambapo zitaenda kucheza ligi daraja la kwanza. https://youtu.be/F5_j1Yh6idc
Attachments area
Preview YouTube video Makamu wa Rais Alaani Mauaji ya Kinyama Mkoani Mwanza Preview YouTube video Serikali Yaombwa Kupeleka Sukari Tandahimba Preview YouTube video Magufuli Akazia Bomba la Mafuta Uganda Tanga Preview YouTube video Serikali Yafanyia Mabadiliko Kanuni Uvunaji Misitu Preview YouTube video Wauguzi Mkoani Tabora Watoa Kero Zao Preview YouTube video Makonda Awataka Wauguzi Kuacha Lugha Chafu Kwa Wagonjwa Preview YouTube video DAWASCO Yamnasa Mwizi Mkubwa Maji Dar Preview YouTube video TPDC Yatangaza Neema Mkoani Lindi Preview YouTube video Benki ya Kilimo Yapania Kukuza Kilimo Nchini Preview YouTube video Serikali Yaombwa Kuongeza Nguvu Sekta ya Utalii Preview YouTube video Mchezo wa Bahati Nasibu Kutimua Vumbi May 24 Preview YouTube video Stand United Nako Kwawaka Moto Preview YouTube video Mashindanon ya Golf Kufanyika Dar Preview YouTube video SHIWATA Kumkabidhi Hekari Zake Samatta Preview YouTube video Chuo Cha Ustawi wa Jamii Wafanya Bonanza Preview YouTube video CAF Yaibeba Yanga, Everton Yafukuza Kocha Preview YouTube video Tani 5000 Za Sukari Zabainika Dar Preview YouTube video Akutwa Na Mifuko Ya Sukari Bila Kibali Preview YouTube video Wananchi Walalamikia Bei Ya Sukari Na Mafuta Preview YouTube video Utaratibu Ufuatwe Kuwasimamisha Kazi Watumishi Preview YouTube video Tanzania Haina Sheria Ya Majenzi Preview YouTube video Wananchi Waelewa Kutumia Mabasi Ya Mwendo Kasi Preview YouTube video Wawekezaji Wa Gesi Wakutana Na Serikali Preview YouTube video Wakulima Waupongeza Mfuko Wa Uzalishaji Korosho Preview YouTube video Wafanyabiashara Walalamikia Ushuru Preview YouTube video Uongozi Yanga Wawapongeza Wachezaji Preview YouTube video Michuano Ya Gofu Kuchezwa Siku Mbili Preview YouTube video Wachezaji Wa Michezo Ya Kubahatisha Watakiwa Kujua Haki Zao Preview YouTube video Mchezo Wa Bao Wakosa Kipaumbele Preview YouTube video Aston Villa New Castle Na Norwich Zashuka Daraja

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.