Mwanamume afariki katika maandamano Kenya



Mwanamume mmoja amefariki wakati wa maandamano ya upinzani katika mji wa Kisumu, magharibi mwa Kenya, watu walioshuhudia wameambia BBC.
Mwanamume huyo anadaiwa kufariki wakati wa makabiliano kati ya polisi na waandamanaji hao wanaowashinikiza maafisa wa Tume ya Uchaguzi (IEBC) kujiuzulu.
Hospitali moja mjini humo imethibitisha kwamba mwili wa mwanamume umefikishwa katika hospitali hiyo lakini chanzo cha kifo chake hakijathibitishwa.
Jijini Nairobi, maafisa wa polisi wametawanya waandamanaji waliokuwa wakitaka kufika katika afisi kuu za tume hiyo.
Shughuli za kibiashara katika jiji hilo zimetatizika pakubwa.
Miji
Image captionMaandamano yameshuhudiwa katika miji mingi mikubwa
Polisi wamekuwa wakikabiliana na makundi ya wafuasi wa muungano huo wa upinzani wa Cord kwa mabomu ya kutoa machozi na maji ya kuwasha.
Maandamano pia yameshuhudiwa katika miji mingine kama vile Mombasa na Kakamega.
Viongozi wa CORD wanasema mmoja wa maseneta wa muungano huo amekamatwa wakati wa maandamano ya leo mjini Kakamega, magharibi mwa Kenya.
Leo imekuwa wiki ya nne ya maandamano hayo ya upinzani.
Wiki iliyopita, polisi walikabili vikali waandamanaji na baadaye walishutumiwa na mashirika ya kutetea haki za kibinadamu kwa kutumia "nguvu kupita kiasi”.
Rais Uhuru Kenyatta wiki jana alisema upinzani unafaa kutumia utaratibu uliowekwa kikatiba iwapo unataka kufanikisha mabadiliko katika tume ya uchaguzi.
Ametoa wito kwa “upinzani kuonesha siasa komavu badala ya kutumia njia haramu kuvutia hisia.”

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.