RAIS DKT SHEIN AFANYA UTEUZI WA WAKUU WA MIKOA NA WILAYA



Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, amefanya uteuzi wa Wakuu wa Mikoa na Wilaya kama ifuatavyo:

1.UTEUZI WA WAKUU WA MIKOA

Uteuzi huo ni kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya kifungu 61(1) cha katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984.

WALIOTEULIWA NI:

I. Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi – Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud.
ii. Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja –Mhe. Vuai Mwinyi Mohammed.

Wakuu wa Mikoa ambao mikoa yao haikutajwa katika taarifa hii wanaendelea na dhamana zao kama kawaida.

2.UTEUZI WA WAKUU WA WILAYA:

Kwa mujibu wa uwezo aliyopewa chini ya kifungu 61(2) cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 , Rais amefanya uteuzi wa Wakuu wa Wilaya kama ifuatavyo:

1. Mkuu wa Wilaya ya Mjini –Mhe. Marina Joel Thomas.
ii. Mkuu wa Wilaya ya Magharibi “B” – Mhe. Silima Haji Haji.
iii. Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini “A” – Mhe. Hassan Ali Kombo.
iv. Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini “B”- Mhe. Issa Juma Ali.
v. Mkuu wa Wilaya ya Kati – Mhe. Mashavu Sukwa Said.
vi. Mkuu wa Wilaya ya Kusini-Mhe. Idrissa Kitwana Mustafa.
vii. Mkuu wa Wilaya ya Chake Chake- Mhe. Salama Mbarouk Khatib.
Aidha Wakuu wa Wilaya ambao wilaya zao hazikutajwa katika taarifa hii, wanaendelea na dhamana zao kama kawaida.

Uteuzi huo unaanza leo Mei 23, 2016.

Viongozi wote hao waliotajwa wanatakiwa waripoti Ikulu mjini Unguja kesho Mei 24, 2016 saa nane za mchana kwa ajili ya kuapishwa.

Taarifa ya mabadiliko hayo imesainiwa na Dk. Abdulhamid Yahya Mzee, ambaye ni Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi, Zanzibar leo 23 Mei, 2016.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI