SAMATTA SASA KUPEWA ENEO JUNI 5



Mwenyekiti wa SHIWATA, Cassim Taalib (aliyesimama) akizungumza na wanachama (hawapo pichani) maandalizi ya sherehe za kumkabidhi eneo mchezaji bora wa Afrika , Mbwana Samatta katika mkutano uliofanyika Dar es Salaam juzi.

MTANDAO wa Wasanii Tanzania (SHIWATA) umesogeza mbele kwa siku moja sherehe za kumkabidhi eneo mchezaji bora wa Afrika, Mbwana Samatta hadi Juni 5, 2016 ili kupisha pambano kati ya Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) na timu ya Taifa ya Misri.

Mwenyekiti wa SHIWATA, Cassima Taalib alisema jana Dar es Salaam kuwa  maandalizi ya sherehe hizo ambazo awali zilipangwa kufanyika Juni 4, 2016 yamekamilika na Mbwana atakabidhiwa hekari tano za eneo ambazo atalitumia kujenga Kituo cha wanamichezo katika eneo la Mwanzega, Mkuranga mkoa wa Pwani.

Alisema hivi karibuni baba mzazi wa mchezaji huyo, Mzee Ali Samatta alishukuru SHIWATA kutambua mchango wa mwanae katika medani ya soka nchini na kuahidi kusaidia kusimamia juhudi za mwanae katika kuendeleza michezo nchini.

Mkurugenzi wa Ufundi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Salum Madadi alithibitisha kufanyika mchezo wa Stars na Misri siku ambayo awali ilipangwa Mbwana kukabidhiwa eneo hilo.

Samatta anayecheza soka ya kulipwa Ulaya atatumia mapumziko ya mechi ya Stars na Misri kukabidhiwa eneo hilo na kadi ya uanachama wa SHIWATA katika kutambua mchango wake kuitangaza Tanzania kuwa mchezaji bora Afrika kati ya wachezaji wanaocheza mpira wa kulipwa ndani ya bara la Afrika.

Katika sherehe hizo wasanii 35 watakabidhiwa nyumba zao kati hiyo, wanachama watatu watakabidhiwa nyumba ndogo, 31 watakabidhiwa misingi na nyumba kubwa moja na kufikia idadi ya nyumba 185 ambazo zimekwisha jengwa kijijini hapo mpaka sasa.

Akizungumza katika mkutano wa wanachama kujiandaa na sherehe hizo walimuomba Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Mnauye awe mgeni rasmi ambapo pia waliomba dua la kumuombea Rais John Pombe Magufuli katika juhudi zake za kupambana na wabadhirifu wa mali ya umma.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*