SHINDANO LA MAISHA PLUS MSIMU WA 5 LAZINDULIWA RASMI, KUONYESHWA MOJA KWA MOJA NA AZAM TV


Mkurugenzi wa Azam Media Tido Mhando (Kushoto) akizungumza wakati wa uzinduzi wa Maisha Plus East Africa Mkurugenzi wa Maisha Plus East Africa msimu wa 5 ambapo shindano linatarajiwa kuanza hivi karibuni itakapotangazwa ratiba ya kutafuta washiriki wa shindano hili mikoani na nchi zingine za Afrika Mashariki, kulia ni mmoja wa waandaji wa shindano hilo Bw. Masoud Kipanya, Masoud Kipanya ni miongoni mwa waanzilishi wa Maisha Plus na mtangazaji wa kipindi hicho ambacho huandaliwa na kampuni ya DMB Company Limited na mwaka huu inandaa kwa udhamini mkubwa wa Azam Media, Hafla ya uzinduzi huo ilifanyika jana katika studio za Uhai Productions – Azam, Tabata jijini Dar es salaam.
Joyce Fisoo Katibu Mtendaji wa bodi ya filamu Tanzania akizungumza mawili matatu wakati wa uzinduzi huo kama mgeni mwalikwa lakini pia kama mdau muhimu wa shindano hilo.
Baadhi ya wageni waalikwa wakiwa katika hafla hiyo
Mmoja wa waandaji wa shindano hilo Bw. David Seburi akizungumza na baadhi ya wageni waalikwa wakati wa hafla hiyo.
Baadhi ya waandaji wa shindano la Maisha Plus kulia Francis Bonga na David Sevuri wakifuatilia matukio wakati wa hafla hiyo iliyofanyika jana.Jikho Man na Vitalis Maembe wakitoa burudani wakati wa hafla hiyo iliyofanyika jana.
Mwandaaji wa shindano hilo Bw. Masoud Kipanya akizungumza na baadhi ya washiriki waliowahi kushiriki katika shindano hilo kulia ni Abdul aliyekuwa mshindi.Aliyewahi kuwa mshindi wa shindano hilo Abdul akizungumza na wageni waalikwa katika uzinduzi huo uliofanyika jana.
Baadhi ya wafanyakazi wa Azam Media wakiwa katika hafla hiyo.
Mwanahabari na Bloger John Bukuku akihojiwa na mtangazaji wa Azam Tv Benerick ambaye pia alikuwa ni mmoja wa washiriki wa msimu uliopita wa Maisha Plus.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

ALLY KAMWE AZIMIA KWA MKAPA.

RAIS SAMIA KUZINDUA MKUTANO MKUU WA 79 WA BARAZA LA MICHEZO YA MAJESHI DUNIANI

MIGINGO KISIWA KIDOGO ZAIDI AFRIKA KILICHOGOMBEWA NA UGANDA, KENYA