MKOA wa Arusha, umefanikiwa kupata madawati 22, 756 na bado una upungufu wa madawati 2577 ili kukamilisha madawati 24,373 ambayo yanahitajika kwa ajili ya shule za msingi za mkoa ambazo hazina madawati.
Hayo yameelezwa na Katibu tawala wa mkoa wa Arusha, Richard Kwitega, wakati wa kuwatunuku vyeti vya madaraja matatu tofauti ya wadau waliochangia madawati kwa kutambua mchango wao katika kuboresha elimu kwenye hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa ofisi ya mkuu wa mkoa..
Kwitega, ambae ametunuku vyeti hivyo kwa niaba ya mkuu wa mkoa, Daud Felix Ntibenda, amesema mkoa huo una jumla ya wanafunzi 285,844 kuanzi darasa la kwanza hadi la saba mwaka 2016, na mahitaji ya Madawati ni 119,765, yaliyokuwepo ni 95,394 .Amewapongezafanyaiashara kwa moyo wao huo na lengo ni kuhakikisha ifikapo julai mosi hakuna mwanafunzi anae kaa chini .
Akikabidhi hati hizo kulingana na mchango uliotolewa na kampuni,Kwitega, amesema serikali inatambua na kuthamini moyo wao wa uzalendo wa kujitolea sehemu ya mapato yao kuchangia madawati kwenye shule za msingi mkoa wa Arusha.
Vyeti hivyo ni vya Fedha, Shaba na Dhahabu, ambapo waliochangia madawati 1 hadi 10,ambao ni 20,wametunukiwa hati a Fedha, waliochangia madawati 11 hadi 19 ,ambao ni 15 wametunukiwa hati za shaba na waliochangia madawati kuanzia 101, na kuendelea ambao ni 5 wametunukiwa hati za dhahabu.
Akizungumza kwenye hafla hiyo mkuu wa mkoa wa Arusha,Daud Felix Ntibenda, amewaomba wafanyabiashara hao kuendelea kuchangia madawati 2577 yanayohitajika ili kukamilisha mahitaji ya mkoa ambayo ni 24,337.
Amesema katika kuhakikisha zoezi hilo linafanikiwa ameunda timu ya wataalamu kwendalaya zote na shule zote ili kujiridhisha kama madawati yanatosheleza au bado kuna upungufu.Ntibenda, amesema Juni 18 ,2016, anaanzisha zoezi la kupita kwenye maduka makubwa na viwanda kwa ajili ya kukusanya madawati yaliyopungua.
Amesema wapo baadhi ya wafanya biashara wakubwa hawajaitikia wito huo hivyo kutumia utaratibu huo wa kuwapitia wataweza kuchangia madawati.
Ntibenda, amesema Julai mosi mwaka huu anaenda kuwsilisha taarifa ya madawati kwa Rais, hivyo hayuko tayari kufukuzwa vkazi kwa kushindwa kufikia malengo ya madawati katika mkoa wakati wapo watu wenye uwezo hawajatoa michango yao.
Ameongeza kuwa ameshakutana na watumishi wa serikali waliopo chini ya ofisi ya Katibu tawala wa mkoa ili nao kila mmoja achangie dawati moja kwa kuwa nao wana watoto waliopo shuleni na tayari amechangia madawati 692.
Comments