MKOA WA ARUSHA WAFANIKIWA KUPATA MADAWATI 22,756 BADO MENGINE 24,373 YAITAJIKA



                     Na Woinde Shizza,Arusha   .
                                                
MKOA wa Arusha, umefanikiwa kupata madawati 22, 756 na bado una upungufu wa madawati 2577 ili kukamilisha madawati 24,373 ambayo yanahitajika kwa ajili ya shule za msingi za mkoa ambazo hazina madawati.

Hayo yameelezwa  na Katibu tawala  wa mkoa wa Arusha, Richard Kwitega, wakati wa kuwatunuku vyeti vya madaraja  matatu tofauti ya wadau waliochangia madawati kwa kutambua mchango wao katika kuboresha elimu kwenye hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa ofisi ya mkuu wa mkoa..

Kwitega, ambae ametunuku vyeti hivyo kwa niaba ya mkuu wa mkoa, Daud Felix  Ntibenda, amesema mkoa huo una jumla ya wanafunzi 285,844 kuanzi darasa la kwanza hadi la saba mwaka 2016, na mahitaji ya Madawati  ni 119,765, yaliyokuwepo ni 95,394 .Amewapongezafanyaiashara  kwa moyo wao huo na lengo ni kuhakikisha ifikapo julai mosi hakuna mwanafunzi anae kaa chini .

Akikabidhi hati hizo kulingana na mchango uliotolewa na kampuni,Kwitega, amesema  serikali inatambua na kuthamini moyo wao wa uzalendo wa kujitolea sehemu ya mapato yao kuchangia madawati kwenye shule za msingi mkoa wa Arusha.

Vyeti hivyo ni vya Fedha, Shaba na Dhahabu, ambapo waliochangia madawati 1 hadi 10,ambao ni 20,wametunukiwa hati a Fedha, waliochangia madawati 11 hadi 19 ,ambao ni 15 wametunukiwa hati za shaba na waliochangia madawati kuanzia 101, na kuendelea ambao ni 5 wametunukiwa hati za dhahabu.

Akizungumza kwenye hafla hiyo mkuu wa mkoa wa Arusha,Daud Felix  Ntibenda, amewaomba wafanyabiashara hao kuendelea kuchangia madawati 2577 yanayohitajika ili kukamilisha mahitaji ya mkoa ambayo ni 24,337.

Amesema katika kuhakikisha zoezi hilo linafanikiwa ameunda timu ya wataalamu kwendalaya zote na shule zote ili kujiridhisha kama madawati yanatosheleza au bado kuna upungufu.Ntibenda, amesema Juni 18 ,2016, anaanzisha zoezi la kupita kwenye maduka makubwa na viwanda kwa ajili ya kukusanya madawati yaliyopungua.

Amesema wapo baadhi ya wafanya biashara wakubwa hawajaitikia wito huo hivyo kutumia utaratibu huo wa kuwapitia wataweza kuchangia madawati.

Ntibenda, amesema Julai mosi mwaka huu anaenda kuwsilisha taarifa ya madawati kwa Rais, hivyo hayuko tayari kufukuzwa vkazi kwa kushindwa kufikia malengo ya madawati katika mkoa  wakati wapo watu wenye uwezo hawajatoa michango yao.

Ameongeza kuwa ameshakutana na watumishi wa serikali waliopo chini ya ofisi ya Katibu tawala wa mkoa ili nao kila mmoja achangie dawati moja  kwa kuwa nao wana watoto waliopo shuleni na tayari amechangia madawati 692.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*