OLE SENDEKA KATIKA AROBAINI YA CHIFU WA WAMASAI


Na Bashir Nkoromo, Kibaha
Msemaji Mkuu wa CCM, Christopher Ole Sendeka, ameongoza shughuli ya arobaini ya Kiongozi wa Jamii ya Wamasai wa kundi la Parakuyo, katika Kanda ya mikoa ya Tanga, Pwani, Morogoro, Mbeya na Iringa, Chifu Moreto Ole Maitei, iliyofanyika leo katika Kijiji cha Kigoda, Kata ya Gwata, Kibaha Vijijini katika mkoa wa Pwani.

Katika shughuli hiyo ambayo ilifanyika kimila, Sendeka ambaye alialikwa kuongoza shughuli hiyo Kama kiongozi wa Kimasai anayeheshimika, aliwataka Jamii ya Wamasai Kanada za mikoa hiyo, kuwa na Umoja na kutumia hekima na busara  katika kumpata mrithi wa nafasi iliyoachwa na Chifu Ole Maitei.

Aliwataka kumteua Chifu au Laiboni, mwenye sifa zinazostahili ambazo hata kama Chifu Ole Maitei angekuwepo angerithika kuwa anafaa kuwa mrithi wake.

Kwa heshima aliyopewa katika shughuli  hiyo Ole Sendeka, aliweka kwenye kaburi kibuyu na usinga ambavyo ni vifaa alivyokuwa akitumia Chifu Ole Maitei ambaye ndani ya Jamii hiyo anatambuliwa zaidi kwa cheo cha Laiboni ambaye ni kiongozi mkuu wa viongozi wanaofuatia hadhi yake wanaoitwa Laigwanani. Uwekaji vifaa hivyo ulifayika huku ukishuhudiwa na ndugu jamaa na wanajamii hiyo, Mjane na Dada wa Marehem.

Mmoja wa Malaigwanani waliohudhuria shughuli hiyo, alisema, Kibuyu hicho alichoweka Ole Sedeka kwenye kaburi, ndani kilikuwa na  mawe ambayo Chifu Ole  Maitei alikuwa akiyatumia kubashiri yanayoweza kutokea mbele ya safari huku usinga akiutumia kupungia kuwasalimia wageni au kufukuzia mbali mifarakano na balaa katika jamii yao.

Kabla ya kuweka vifaa hivyo kwenye kaburi, Sendeka alitanguliwa na watoto wote wa kiume kumwaga kwenye kaburi hilo  asali, maziwa ya ng'ombe na mafuta ya kidari cha dume maalum la ng'ombe kama ishara ya kutekeleza mila na desturi.

Chifu  Ole Maitei ambaye alikuwa kiungo muhimu kwa kuunganisha jamii hiyo ya Kimasai  hasa katika utatuzi wa migogoro yawafugaji kutoka jamii hiyo na wakulima katika maeneo mbalimbali ya mikoa ya Tanga, Pwani, Morogoro, Mbeya na Iringa alipokea nafasi ya Uchifu kutoka kwa Laibon Labani Moreto ambaye alifariki miaka ya 2005. PICHA KEM KEM ZA TUKIO HILO>BOFYA HAPA

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.