Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli
akihutubia kwenye uzinduzi wa kituo cha Mawasiliano cha Polisi Call
Centre Biafra Kinondoni.
Jonas Kamaleki, MAELEZO
Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli
amelitaka jeshi la polisi nchini kuwadhibiti majambazi ipasavyo kwa
kuwanyanganya silaha kwenye matukio ya kiuharifu ili kukomesha vitendo
viovu katika Taifa.
Rais Magufuli ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa Mpango wa Usalama wa Jamii.
“Inashangaza
jambazi anavamia kituo cha polisi anaua na anaondoka wakati polisi wapo
na wana silaha na risasi wanazo lakini wanashindwa kumnyang’anya
silaha,”alishangaa Rais Magufuli.
Ameongeza
kuwa ujambazi na vitendo vya uharifu nchini inabidi vikomeshwe mara
moja ili watanzania waishi kwa amani na kufanya maendeleo kwani wananchi
wanataka maendeleo.
Akiongelea
kuhusu maslahi na vitendea kazi kwa jeshi la polisi, Rais Magufuli
amesema kuwa serikali yake itafanya kila iwezalo kuliwezesha jeshi hilo
ili liweze kufanya kazi kwa ubora zaidi.
Rais
Magufuli ameonyesha kuwa na imani na jeshi la polisi licha ya kuwa na
kasoro ndogo ndogo kwa baadhi ya polisi ambao wanalichafua jeshi hilo.
Aidha
ametoa agizo kwa TCRA kushirikiana na jeshi la polisi nchini ili kuweza
kurekodi simu na kutoaprint out mara moja tofauti na ilivyo sasa.
Kuhusu
kundi la wafanyakazi wanaofanyakazi kwenye Dawati la Taarifa la polisi,
Mhe. Rais amemtaka Mkuu wa Jeshi hilo, IGP Ernest Mangu kuwafikiria na
kuwapatia posho ya kazi kwani kazi wanayoifanya ni ngumu mno na
inahitaji umakini zaidi.
Kwa
upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amemwomba Mhe.
Rais kuliongezea fedha jeshi hilo ili liweze kufanya kazi kwa ustadi
zaidi na kukomesha vitendo vya uharifu nchini.
Makonda amelipongeza jeshi la polisi kwa kudhibiti matukio ya ujambazi hapa nchini hususan kwenye mabenki.
Mpango
huu wa Usalama wa Jamii umezinduliwa leo na utadumu hadi 2019 na
unatarajiwa kutoa matokeo makubwa ya kudhibiti uharifu nchini.
Comments