MALINZI AMPONGEZA MANJI KWA USHINDI YANGA




              TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - RELEASE NO. 122                                                                                       TAREHE JUNI 12, 2016


MALINZI AMPONGEZA MANJI, YANGA

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amempongeza Yussuf Manji kwa kuchaguliwa tena kuwa Mwenyekiti wa Young Africans SC baada ya kupata kura 1,468 kati ya 1,470 zilizopigwa. Kura mbili ziliharibika kwa nafasi hiyo.

Kadhalika Rais Jamal Malinzi amempongeza Clement Sanga kwa kuchaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti  baada ya kupata kura 1,428 wakati mpinzani wake Titus Osoro alipata kura 80. Kura 1,508 zilipigwa katika nafasi ya kuwania makamu mwenyekiti.

Kadhalika wajumbe wanane wanaounda Kamati ya Utendaji kwa kuchaguliwa kuongoza Klabu ya Young Africans kwa miaka minne ijayo kwa mujibu wa katiba.
Wajumbe waliochaguliwa ni Omary Said (1,069), Siza Lyimo (1,027), Salum Mkemi (894), Thobius Lingalangala (889), Ayoub Nyenzi ((889), Samwel Lukumay (818), Hussein Nyika (770) na Hashim Abdallah (727.

Katika salamu hizo za pongezi, Rais Jamal Malinzi pia amewapongeza wanachama wa Young Africans kwa kufanya uchaguzi wa amani na utulivu.

Kutokana na hali hiyo, Rais Jamal Malinzi amewataka uongozi huo wa Young Africans kufungua ukurasa mpya wa kuendesha klabu hiyo na kuiletea mafanikio klabu hiyo kongwe na maarufu katika ukanda wa nchi za Afrika Mashariki na Kati hasa wakati huu ambako Young Africans inashiriki hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika (CAFCC).

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

𝙂𝘼𝙈𝙊𝙉𝘿𝙄 𝙆𝘼𝘾𝙃𝙀𝙕𝘼 𝙆𝙄𝘽𝙄𝙉𝙂𝙒𝘼.