WAZAZI WATAKIWA KUWAJENGEA WATOTO WAO TABIA YA KUPENDA MICHEZO


 Meneja wa bank ya CRDB tawi la Usa River wilayani Arumeru mkoani arusha akimlisha keki moja ya mtoto alieshiriki katika maadhimisho ya siku ya mtoto Africa iliyoandaliwa na bank hiyo katika viwanja vya Usa River Academy.

Watoto wakishandana kukimbia katika siku ya mtoto wa Africa iliyoandaliwa na bank ya CRDB tawi la Usa River wilaya ya Arumeru mkoania Arusha katika viwanja vya usa river academy.




 Watoto wakishandana kukimbiza kuku katika michezo iliyoandaliwa na bank ya CRDB tawi la Usa River wilayani Arumeru mkoani Arusha hivi karbuni katika michezo ya kuazimisha siku ya mtoto wa Africa iliyofanyika katika viwanja vya shule ya Usa River Academy.
Watoto wakishandana kukimbia na magunia  katika siku ya mtoto wa Africa iliyoandaliwa na bank ya CRDB tawi la Usa River wilaya ya Arumeru mkoania Arusha katika viwanja vya usa river academy


Na Woinde Shizza,Arusha

Benki ya CRDB tawi la Usariver imewahimiza wazazi na walezi kujenga tabia ya kuwaendeleza watoto katika michezo na vipaji walivyonavyo ili viweze kuwaimarisha kiakili na kimwili na kuwanufaisha baadae.

Meneja wa Tawi  hilo Jenipher Tondi  ameyasema hayo katika michezo ya watoto iliyoandaliwa na benki hiyo katika viwanja vya USARIVER ACADEMY ambapo watoto walipata fursa ya kucheza michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu,netiboli,kukimbiza kuku na mbio za kukimbiza magunia..

Amesema kuwa wazazi hawana budi kuendeleza vipaji vya watoto kwani vinaweza kuwa na faida kwa familia,jamii na taifa. “wazazi wawape watoto nafasi ya kushiriki katika michezo ili kuweza kuvumbua vipaji vyao vilivyojificha sababu vipaji ni ajira tosha”
Pia amewakumbusha wazazi kuwawekea watoto akiba ya fedha kwa ajili ya kumsaidia mtoto katika kulipa fedha za ada kwa kufungulia account zisiszo kuwa na riba.

Kwa upande wao watoto walioshiriki katika michezo hiyo Oscar Damian na Angela John wameishukuru benki hiyo kwa kuwajali na kuwapa nafasi ya kukutana na watoto wenzao ambapo wameweza kuburudika na michezo iliyoandaliwa.

Jane Nassari amewataka wazazi kujenga utamaduni wa kuwaruhusu watoto wao kushiriki kwenye michezo kwasababu michezo huleta afya ya akili,furaha na mashirikiano.

Mzazi aliyefika katika siku hiyo Angelina Joseph  amesema kuwa mazingira bora ya michezo yanapaswa kujengwa ili watoto wapende michezo na kunufaika nayo kwa kuitumia kama njia ya kujiimarisha kiafya na kiakili.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA