MKWASA AAHIRISHA KAMBI TAIFA STARS
Kutokana na maombi ya klabu nyingi za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kutaka kuandaa wachezaji kwa ajili ya Ligi Kuu msimu unaoanza sasa, umemlazimu Kocha Mkuu timu ya Mpira Tanzania ‘Taifa Stars’, Charles Boniface Mkwasa kuahirisha kambi iliyokuwa ianze Jumatatu Agosti mosi, mwaka huu, imefahamika.
Wachezaji ambao Mkwasa amewaita wanatoka kwenye klabu mbalimbali na ambazo zinaongoza kutoa nyota wengi ni Simba SC, Young Africans SC, Azam FC na Mtibwa Sugar FC.
Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini
MAKOCHA TANZANIA WAANZA KUIVA
Makocha 20 wa Tanzania wanaofanya kozi ya Leseni A kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), wamemaliza kozi hiyo hatua ya kwanza na kusema, “Tumenolewa na sasa tumeiva vya kutosha,” amesema mmoja wa wanafunzi hao, Wilfred Kidao leo saa Julai 30, 2016 wakati Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi.
Kidao amesema japo kozi hiyo ilikuwa hatua ya kwanza ‘Module 1’ kwa sasa wameiva kiasi kwamba watakapomaliza Novemba, mwaka huu wana uhakika wa kupeleka vyeti vyao sehemu yoyote duniani kuomba kazi na kushinda kwa kuwa wameiva vilivyo. Wakufunzi wa kozi hiyo walitokea CAF, Sunday Kayuni na Salum Madadi ambaye ni Mkurugenzi wa Ufundi wa TFF.
Kwa taarifa zaidi, fuata link hapo chini
Comments