MAKAMU WA RAIS AZINDUA MRADI WA GREEN VOICES



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa uzinduzi wa  Mradi wa Green Voices Tanzania uliofanyika katika hoeteli ya Serena jijini Dar es Salaam

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipata maelezo namna ya mkaa wa karatasi unavyofanya kazi kutoka kwa Mkurugenzi wa kampuni ya Mchau Windmill Ndugu Laurian Mchau wakati wa uzinduzi wa mradi wa Green Voices Tanzania
 Keki ya Muhogo
 Mkaa wa karatasi
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassanakipata maelekezo ya namna zao la muhogo linavyoweza kuwa na idadi nyingi ya vyakula.
Mshauri na Mjumbe wa Bodi ya Mfuko wa Wanawake Barani Afrika Mhe. Getrude Mongella akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi wa Green Voices Tanzania uliozindiliwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe. Samia Suluhu Hassan.
                                                  ...........................


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewahimiza watendaji wa Mradi wa Jukwaa la Kijani la wanawake Nchini wahakikishe wanaendelea na mkakati wa kuelemisha wanawake kuhusu namna ya kukukabiliana na mabadiliko ya Tabia hapa Nchi.


Makamu wa Rais SAMIA SULUHU HASSAN ametoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam wakati anazindua mradi wa GREEN VOICES,mradi unaolenga kusaidia wanawake kukabiliana na mabadiliko ya Tabia,unaofadhiliwa na Rais wa Mfuko wa Wanawake Barani Afrika Maria Tereza Fernandes De la Vega

Makamu wa Rais pamoja na kupongeza jitihada zinazofanywa na Jukwaa hilo katika kusaidia wanawake kupambana na mabadiliko ya Tabia ya nchini, amesema bado upo umuhimu mkubwa kwa wanawake kuelimishwa  zaidi kuhusu mabadiliko hayo kwa sababu wao ni moja ya kundi ambalo linaguswa na mabadiliko ya tabia ya nchi ikiwemo suala la ukame.

Amesema bara la Afrika linapoteza mabilioni ya dola kutokana na mabadiliko ya Tabia ya Nchi ikiwemo tatizo la ukame ambao umechangia kupunguza uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara kwa kiasi kikubwa pamoja na uhaba wa maji.
Makamu wa Rais SAMIA SULUHU HASSAN amesema nchi za Afrika bado zinakabiliana uhaba wa kifedha,taarifa sahihi na teknolojia  katika jitihada za kupambana ipasavyo na mabadiliko ya tabia ya nchini.
 


BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI

KOCHA WA AL.AHLY ASEMA YANGA NI TIMU BORA NA NGUMU