Mdunguaji amewapiga risasi na kuwauwa polisi wanne na kujeruhi wengine saba huko Dallas, Marekani katika maandamano ya kupinga mauaji ya watu weusi yanayofanywa na polisi.Milio ya risasi ilisikika wakati waandamanaji walipokuwa wakiandamana katika mji huo. Mtu mmoja anashikiliwa na polisi na mwingine mmoja aliyeonekana na bunduki amejisalimisha.
Hali ilikuwa inatisha kiasi ya watu kujificha kwenye magari wakati polisi wakihaha kumsaka mdunguaji
Huyu aliamua kundamana na bunduki yake, na sasa amejisalimisha polisi kwa mahojiano zaidi.
Comments