WADAU WA MAAFA WAJENGEWA UWEZO KUANDAA KANZI DATA YA ATHARI ZA MAAFA.


g1Mratibu wa Maafa Shirika la Umoja wa Mataifa la Upunguzaji Athari za Maafa (UNISDR) Bw.Adam Fysh akielezea jambo wakati wa mafunzo ya kuandaa Kanzi Data ya Masuala ya Athari za Maafa yaliyofanyika tarehe 19 na 20 Julai, 2016 katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu.
g2g3Baadhi ya wadau wa masuala ya maafa wakifuatilia maelezo kutoka kwa Mratibu wa Maafa Shirika la Umoja wa Mataifa la Upunguzaji Athari za Maafa (UNISDR) Bw.Adam Fysh (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya kuandaa Kanzi Data ya Athari za Maafa nchini yaliyofanyika kuanzia tarehe 19-20 Julai, 2016 katika Ukumbi wa Mikutano Ofisi ya Waziri Mkuu.
g4Mratibu wa Maafa Shirika la Umoja wa Mataifa la Upunguzaji Athari za Maafa (UNISDR) Bw.Adam Fysh akitoa ufafanuzi kwa kikundi ‘A’ cha majadiliano wakati wa mafunzo ya kuandaa Kanzi Data ya Athari za Maafa yaliyofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu Julai 19 na 20, 2016.
g5Mkurugenzi wa Idaya ya Uratibu wa Maafa Ofisi ya Waziri Brig. Jenerali, Mbazi Msuya (katikati mwenye tai nyekundu) akiwa katika picha ya pamoja na wadau wa masuala ya maafa mara baada ya ufunguzi wa mafunzo ya kuandaa Kanzi Data ya Athari za Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu, kulia kwake ni Mratibu wa Maafa Shirika la Umoja wa Mataifa la Upunguzaji Athari za Maafa (UNISDR) Bw.Adam Fysh.
(PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)
…………………………………………………………………………………………….
Na. MWANDISHI WETU
Shirika la Umoja wa Mataifa la Upunguzaji Athari za Maafa (UNISDR) kwa kushirikiana na Idara ya Uratibu wa Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu wameendesha mafunzo ya siku mbili kwa wadau wa masuala ya maafa juu ya namna ya kutumia Kanzi Data ya takwimu za Athari za Maafa kutoka Wizara na Taasisi za Serikali nchini.
Mafunzo hayo yalifanyika Julai 19 na 20, mwaka huu katika Ofisi ya Waziri Mkuu na kushirikisha Wizara na Taasisi za Serikali ikiwemo; Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Wizara ya Ulinzi na Usalama wa Taifa, Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, Jeshi la Zima Moto, Jeshi la Polisi, Mamlaka ya Hali ya Hewa, Mamlaka ya Usafiri wa Majini na Nchi Kavu, TAMISEMI, Chuo Kikuu cha Ardhi, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Ofisi ya Taifa ya Takwimu.
Mafunzo hayo yalijikita katika kusaidia wadau wa masuala ya maafa katika kuongeza uwezo wa kuwa na Takwimu sahihi za majanga yanayoikabili Nchi ya Tanzania.
Akizungumza wakati wa Mafunzo hayo Mratibu wa Masuala ya Maafa Shirika la Umoja wa Mataifa la Upunguzaji Athari za Maafa, Bw. Adam Fysh alieleza kuwa, Mafunzo hayo yatasaidia kuongeza uboreshaji wa kumbukumbu za maafa nchini, “kama ilivyokusudiwa, mafunzo yatasaidia kuwa na rekodi za kutosha, yatasaidia ufuatiliaji, kuwa na tathimini za mara kwa mara, na ulinganifu wa kujua nchi zingine zinafanya nini katika kukabiliaana na athari za maafa, mafunzo haya pia yatasaidia wahusika kufanya maamuzi sahihi na kwa wakati katika maendeleo hususani kwa kupunguza athari za maafa hapa nchini”
Bw. Fysh aliongeza kuwa kiu yake ni kuona nchi zinajikita katika utoaji wa taarifa zenye uhalisia na sahihi ili kuwa na kumbukumbu na takwimu zenye kusaidia Dunia kujua maafa yanayotokea, “Natamani kuona tunakuwa na takwimu sahihi na zenye mpangilio zinazohusu athari za maafa hususani yanayoikabili nchi’
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Idaya ya Uratibu wa Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu  Brig. Jenerali, Mbazi Msuya alishukuru jitihada za Shirika hilo kwa kuona umuhimu wa kuwajengea uwezo wadau wa masuala ya Maafa na kueleza kuwa mafunzo hayo yamekuja kwa wakati na yataleta manufaa makubwa kwa Taifa.
“Nawapongeza Shirika kwa kuona ni vyema kuifikia Tanzania kwa kuijengea uwezo wa namna ya kuweka taarifa muhumu za masuala ya Maafa katika kanzi data. Hii itatusaidia sana katika kupanga mipango yetu kwa namna bora zaidi na vile vile itarahisha katika kufuatilia kufanya tathmini”, Alisema Brig. Msuya
Naye Mtaalam wa Masuala ya Hali ya Hewa kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa, Bi.Hellen Msemo alieleza kuwa mafunzo hayo yatasaidia kutoa fursa za kimaendeleo kwakuwa takwimu za athari za maafa zitasaidia kuwa na mipango mizuri ya maendeleo ya nchi na kuipongeza Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kuona umuhimu wa kuratibu mafunzo hayo.
Mafunzo ya kutumia Kanzi Data ya takwimu za Athari za Maafa tayari yamezifikia nchi 31 duniani huku Tanzania ikiwa ni miongoni mwa nchi kumi na tatu za Afrika zilizonufaika na elimu hiyo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI

KOCHA WA AL.AHLY ASEMA YANGA NI TIMU BORA NA NGUMU